Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 14 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 182 2024-04-25

Name

Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza:-

Je, lini Serikali itakamilisha kusambaza umeme wa REA kwenye vijiji 20 vilivyobaki – Mkalama?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, Jimbo la Mkalama lina vijiji 70 na vyote vimepatiwa umeme, vikiwemo vijiji 25 vilivyokuwa katika Mradi wa Kusambaza Umeme, Awamu ya Tatu, Mzunguko wa Pili, uliotekelezwa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA). Aidha, Jimbo hilo lina vitongoji 388 ambapo vitongoji 192 vimepatiwa umeme na vitongoji 196 bado havijapatiwa umeme. Katika mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali kupitia REA imetenga fedha za kutekeleza mradi wa kupeleka umeme kwenye vitongoji 15 vya kila jimbo ikiwemo Jimbo la Mkalama. Kwa sasa, REA inakamilisha taratibu za kuwapata Wakandarasi watakaotekeleza mradi huu. Vitongoji vitakavyobakia vitapatiwa umeme kulingana na upatikanaji wa fedha.