Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha kusambaza umeme wa REA kwenye vijiji 20 vilivyobaki – Mkalama?

Supplementary Question 1

MHE. JESCA D. KISHOA: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nishukuru Serikali kwa kutupatia umeme kwenye vijiji vyote 70, lakini changamoto kubwa iliyopo ni size ya transformer zilizofungwa. Wamefunga size ya transformer kVA 50 na mahitaji ni makubwa, wananchi wana viwanda vya alizeti na viwanda vya kuchomelea. Swali la kwanza; je, Serikali haioni kuna haja ya kufunga transformer za kVA 200 mpaka 345 ili kupata umeme wa uhakika?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; nimesikia Serikali kwamba wako kwenye hatua za kutafuta wakandarasi kwa ajili ya kutengeneza kwenye vitongoji. Kumekuwa kuna kasumba miaka yote ya kupata wakandarasi wasiokuwa na sifa. Nataka kujua Serikali wamejipanga vipi kuhakikisha katika eneo la due diligence hawafanyi makosa? Nakushukuru. (Makofi)

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ahsante, tumepokea maoni ya Mheshimiwa Mbunge na maoni ya Waheshimiwa Wabunge wengi na kwa hivyo tumefanyia kazi, kuanzia mwaka huu unaokuja wa fedha 2024/2025, tutaongeza ukubwa wa transformer. Zitakuwepo transformer za ukubwa wa KVI 50, KVI 100 na KVI 200 na zitafungwa kulingana na mahitaji ya eneo husika. Namhakikishia Mheshimiwa Mbunge, jambo hilo tumelipokea na lipo tayari kwenye utekelezaji.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na wakandarasi wanaosuasua kwenye miradi; maelekezo ya Serikali, kupitia Mheshimiwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, yalishatoka. Hatutawavumilia wakandarasi wote wanaotekeleza miradi kwa kusuasua na kutoendelea mbele, kupitia Taasisi zetu za TANESCO na REA hatutawapatia kazi wakandarasi wanaosuasua katika miradi yetu, ahsante.

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha kusambaza umeme wa REA kwenye vijiji 20 vilivyobaki – Mkalama?

Supplementary Question 2

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Spika, ahsante, Wilayani Rungwe vijiji saba mpaka sasa hivi havijafikiwa na umeme wa REA. Vijiji hivyo ni Mpindo, Kata ya Bulyaga; Isumba Kata ya Kinyala; Kyobo Juu, Kata ya Ikuti; Ngumbulu, Kata ya Isongole; Mpombo, Kata ya Lupepo; Isabula, Kata ya Kisiba; na Kasanga, Kata ya Mpombo. Je, ni lini vijiji hivyo vitapata umeme wa REA? Ahsante.

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, nimwambie Mheshimiwa Mbunge, katika vijiji vyote hivi saba vilivyopo katika Jimbo la Rungwe mkandarasi yuko site. Namhakikishia kwamba, tutaongeza usimamizi kuhakikisha vijiji hivi vinapatiwa umeme kulingana na mikataba yetu ambayo ni Juni, mwaka huu. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge, tutasimamia vizuri na tutahakikisha wananchi wa Jimbo la Rungwe wanapata umeme katika vijiji hivi saba, ahsante.

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha kusambaza umeme wa REA kwenye vijiji 20 vilivyobaki – Mkalama?

Supplementary Question 3

MHE. FRANCIS I. MTINGA: Mheshimiwa Spika, naishukuru Serikali kwa kumaliza kuweka umeme katika vijiji vyote 70 vya Mkalama. Naomba commitment ya Serikali kuhusu vitongoji 15 ambavyo nimeviombea umeme, ni lini umeme utawashwa? Ahsante.

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, vitongoji hivi 15 katika Jimbo la Mkalama na katika majimbo yote, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge na ninalitaarifu Bunge lako Tukufu kuwa, tupo katika hatua za manunuzi. Namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kuwa, hivi karibuni tutakamilisha na tutaenda kwenye utekelezaji wa kupeleka umeme kwenye vitongoji 15 katika kila jimbo, ahsante.

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha kusambaza umeme wa REA kwenye vijiji 20 vilivyobaki – Mkalama?

Supplementary Question 4

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Spika, je, ni lini Serikali itasambaza umeme kwa bei ya vijiji katika Kata ya Katindiuka, kama ilivyokuwa imeahidi?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, katika maeneo yote ambayo tunatekeleza miradi ya kupeleka umeme vijijini bei ya kuunganisha umeme ni 27,000. Katika maeneo ya vijiji-miji ambako bei ni zaidi ya hiyo, tunaendelea kufanya mkakati wa kuona namna ambavyo tunaweza tukaenda kwa ajili ya ku-incorporate hata wananchi ambao hawana uwezo wa kulipa 321,000, lakini katika maeneo yote tunayotekeleza miradi yetu ya vijiji bei ya kuunganisha umeme ni 27,000 na tutaendelea kufanya hivyo, ahsante.

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha kusambaza umeme wa REA kwenye vijiji 20 vilivyobaki – Mkalama?

Supplementary Question 5

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, je, ni lini Serikali itamaliza kusambaza umeme katika vijiji vilivyobaki katika Mkoa wa Singida?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, katika vijiji ambavyo vimebakia katika Mkoa wa Singida wakandarasi wanaendelea na kazi ya kufikisha umeme kwenye vijiji hivyo. Namhakikishia Mheshimiwa Mbunge tutaendelea kusimamia kwa weledi mkubwa sana ili vijiji vilivyobakia viweze kupata umeme kwa wakati. Ahsante.