Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 14 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 184 2024-04-25

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:-

Je, lini Serikali itapeleka fedha na wataalam katika eneo la Mbongo, Kata ya Manda ambalo linafaa kwa ufugaji wa samaki kwenye vizimba?

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba katika ziwa ni lazima kuzingatia vigezo vya kisheria na kitaalam, ikiwemo kufanya tathmini ya kimkakati ya mazingira (Strategic Environmental Assessment). Aidha, katika mwaka wa fedha 2023/2024, kupitia Progaramu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo (ASDP II), Serikali imetenga kiasi cha shilingi 233,500,000 kwa ajili ya kuiwezesha Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi (TAFIRI) kufanya tathmini ya kimkakati ya mazingira, ambayo ni takwa la kisheria katika Ziwa Tanganyika na Ziwa Nyasa yakiwemo maeneo ya Manda ili kutambua maeneo yanayofaa kwa ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba.

Mheshimiwa Spika, baada ya tathmini kukamilika, maeneo yatakayobainika kuwa yanafaa kwa ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba yataingizwa kwenye Bajeti na Mpango wa Wizara wa mwaka wa fedha 2024/2025 ili kuwezesha upatikanaji wa fedha na wataalam katika eneo hilo, ahsante.