Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka fedha na wataalam katika eneo la Mbongo, Kata ya Manda ambalo linafaa kwa ufugaji wa samaki kwenye vizimba?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, naipongeza Taasisi ya Uvuvi na Utafiti kwa kuweza kuendelea na mchakato wa kubaini maeneo yanayofaa kwa ajili ya ufugaji wa samaki wa vizimba. Swali langu la kwanza; ni lini Serikali itamaliza mchakato huo ili wananchi wa Ludewa wapate fursa ya kuendelea na biashara hiyo?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; Wizara ina mkakati gani wa kufanya utafiti katika maeneo ambayo ni mazalia ya samaki kwa lengo la kuhifadhi na kufanya samaki waendelee kuwa wengi katika Ziwa Nyasa? Ahsante. (Makofi)

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika jibu la msingi kwamba, tumepokea concern ya Mheshimiwa Mbunge, tutaiweka katika bajeti ya 2024/2025 ili kwenda kufanya tathmini katika eneo hilo analolizungumza Mheshimiwa Mbunge.

Mheshimiwa Spika, hili la pili, namna gani ya kuongeza uzalishaji wa samaki; kama nilivyosema katika majibu ya msingi kwamba, Serikali sasa imekuja na mpango wa vizimba na tunazidi kuhamasisha wavuvi wajikite zaidi katika vizimba kwa sababu, uvuvi huu wa sasa umebadilika duniani kote, kwamba sasa tunakwenda katika hali ya kutengeneza vizimba ili kuleta tija zaidi katika uzalishaji wa samaki.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu katika Maziwa yetu yote makubwa Nyasa, Victoria na Tanganyika, ukweli ni kwamba, mazalia ya samaki yanapotea kwa sababu ya wingi wa watu na uvuvi haramu. Kwa hiyo, ni lazima tuje na mkakati mpya ambao utawezesha watu wetu kuendelea na uvuvi wa kisasa zaidi, hasa kwenye vizimba, ahsante.