Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 41 2024-04-05

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga soko la kisasa Singida Mjini kwani Soko Kuu la Ipembe ni la muda mrefu na miundombinu yake ni chakavu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kuwa miundombinu ya Soko Kuu la Singida Mjini lililopo Mtaa wa Ipembe ni ya muda mrefu na ni chakavu. Halmashauri ya Manispaa ya Singida iliandaa andiko la kuomba fedha za ujenzi wa Soko la Vitunguu la Misuna na Soko Kuu la Ipembe ambalo limependekezwa kujengwa upya.

Mheshimiwa Spika, kupitia Mradi wa Tanzania Cities Transforming Infrastructure and Competitiveness (TACTIC) unaofadhiliwa na Benki ya Dunia Soko la Vitunguu la Misuna lilipata ufadhili kwa awamu ya kwanza na shughuli za upembuzi na usanifu wa mradi zinaendelea. Kwa upande wa Soko Kuu la Ipembe, Mkandarasi anatazamiwa kuanza utekelezaji wa mradi ifikapo Disemba, 2024. Ahsante.