Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga soko la kisasa Singida Mjini kwani Soko Kuu la Ipembe ni la muda mrefu na miundombinu yake ni chakavu?

Supplementary Question 1

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, naomba niulize swali dogo moja la nyongeza. Serikali imejipanga vipi kuhakikisha wakati wa ujenzi wa Soko hili jipya la Ipembe kwamba shughuli za wafanyabiashara hazitaathirika?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, katika taratibu za ujenzi wa miradi hii na hususani miradi ambayo tayari wananchi wanafanyia shughuli zao za kiuchumi katika maeneo hayo, utaratibu utazingatiwa kwa kushirikisha wananchi wenyewe lakini pia Viongozi wa Halmashauri. Mheshimiwa Mbunge tutashirikiana na Ofisi ya Rais, TAMISEMI kuona ni namna gani tunawawezesha wananchi wale kuendelea na shughuli zao bila kuathirika lakini pia hilo soko linajengwa. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga soko la kisasa Singida Mjini kwani Soko Kuu la Ipembe ni la muda mrefu na miundombinu yake ni chakavu?

Supplementary Question 2

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Je, Serikali ina mpango gani wa kuliboresha Soko la Stereo Temeke liendane na ukuaji wa Mji wa Temeke?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Ofisi ya Rais, TAMISEMI tumekwishafanya tathmini ya masoko makubwa ya kimkakati katika halmashauri zetu zote ikiwemo Halmashauri ya Temeke katika Soko lile la Stereo. Tayari Serikali imeshaweka mpango kwanza kupitia mapato ya ndani ili ianze kutengwa fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wakati Serikali Kuu inatafuta fedha kwa ajili ya kuunga mkono juhudi hizo. Kwa hiyo, naomba nitumie fursa hii kumwelekeza kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke kuweka kipaumbele katika bajeti zake ili tuanze kuboresha Soko la Stereo. Ahsante sana.

Name

Gibson Blasius Meiseyeki

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga soko la kisasa Singida Mjini kwani Soko Kuu la Ipembe ni la muda mrefu na miundombinu yake ni chakavu?

Supplementary Question 3

MHE. MAIMUNA A. PATHAN: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Je, ni lini Serikali itajenga soko zuri katika Wilaya ya Nachingwea kwa sababu lililopo limechakaa sana?

Name

Gibson Blasius Meiseyeki

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arumeru-Magharibi

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, lengo la Serikali ni kujenga masoko mazuri ili kuboresha huduma kwa wananchi likiwemo soko hili katika Halmashauri ya Nachingwea. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge amekuwa akishirikiana na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Nachingwea na niwahakikishie tu kwamba tumeshamwelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nachingwea kufanya tathmini ya gharama zinazohitajika kujenga soko lile ili tuweze kuona tunapata fedha kupitia mapato ya ndani na Serikali Kuu kwa ajili ya kuboresha soko hilo. Ahsante.

Name

Mariam Madalu Nyoka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga soko la kisasa Singida Mjini kwani Soko Kuu la Ipembe ni la muda mrefu na miundombinu yake ni chakavu?

Supplementary Question 4

MHE. MARIAM M. NYOKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Je, ni lini Serikali itajenga Soko la Manzese lilipo Kata ya Misufini, Manispaa ya Songea? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, Soko hilo la Manzese lililoko Manispaa ya Songea linamilikiwa na Halmashauri na tulishaelekeza Halmashauri kupitia Wakurugenzi na Menejimenti ya Halmashauri kufanya tathmini na kuweka vipaumbele vya masoko. Kwa hiyo, naomba nilichukue suala hili la Mheshimiwa Mbunge na baada ya kikao hiki tutawasiliana na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea ili tuweze kujua status ya utekelezaji ikoje na tuweze kuona namna gani tunapata fedha kwa ajili ya kuboresha soko hilo. Ahsante.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga soko la kisasa Singida Mjini kwani Soko Kuu la Ipembe ni la muda mrefu na miundombinu yake ni chakavu?

Supplementary Question 5

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Spika, je, ni lini Serikali itajenga soko jipya Wilayani Lushoto maana lililopo ni la tangu mkoloni? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, soko ambalo linahitajika katika Halmashauri ya Lushoto ni moja ya vipaumbele vya Serikali, kazi kubwa ambayo inafanywa ni halmashauri zenyewe kufanya tathmini ya gharama zinazohitajika kulingana na design ya masoko yenyewe.

Mheshimiwa Spika, nitumie nafasi hii kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI kuwaelekeza Wakurugenzi wote wa Manispaa, Halmashauri na Majiji kote nchini kuhakikisha kwanza wanafanya tathmini ya uhitaji wa masoko hayo, lakini pia kuandaa makadirio ya gharama na kuanza kutenga fedha za mapato ya ndani kwa awamu wakati huo na kuwasilisha Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa ajili ya kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa masoko hayo kwa awamu. Nakushukuru sana.

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga soko la kisasa Singida Mjini kwani Soko Kuu la Ipembe ni la muda mrefu na miundombinu yake ni chakavu?

Supplementary Question 6

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa kuwa shughuli ya kiuchumi katika Halmashauri ya Wilaya ya Rorya ni pamoja na uvuvi wa samaki na dagaa lakini hatuna soko la kisasa. Je, ni lini Serikali itajenga soko la kisasa kwa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba katika maeneo ya uvuvi tunahitaji kuwa na masoko ya kisasa ya samaki na hicho ni kipaumbele cha Serikali. Nimwombe Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa sababu tulishafanya ziara pale Halmashauri ya Rorya na miongoni mwa eneo ambalo tulipita ni pamoja na maeneo ya masoko. Nimhakikishie tu kwamba Serikali inaendelea kutafuta fedha ili twende kujenga Soko la Kisasa la Samaki katika eneo hilo la Rorya. Ahsante.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga soko la kisasa Singida Mjini kwani Soko Kuu la Ipembe ni la muda mrefu na miundombinu yake ni chakavu?

Supplementary Question 7

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa hii nafasi. Je, Serikali imefikia hatua gani katika mchakato wa kujenga Soko la Kisasa katika eneo la Madira ambalo michoro yake tumeshawasilisha Wizarani? Nashukuru sana.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, kwanza niipongeze Halmashauri ya Meru kwa kupitia Mheshimiwa Mbunge Pallangyo kwa kuandaa michoro na kuwasilisha Ofisi ya Rais, TAMISEMI kama maelekezo ya Serikali yalivyopelekwa. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba sasa tutafanya tathmini kuona gharama hizo zinazohitajika na kuona vyanzo vya fedha kupitia Serikali Kuu, lakini pia kupitia mapato ya ndani ili tuanze kujenga soko hilo kwa awamu. Ahsante.

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga soko la kisasa Singida Mjini kwani Soko Kuu la Ipembe ni la muda mrefu na miundombinu yake ni chakavu?

Supplementary Question 8

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Masasi haina soko kabisa, ni lini Serikali itajenga soko katika Kijiji cha Mbuyuni? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, kwanza nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Lulindi kwamba Serikali ilikwishatoa maelekezo kwa Wakurugenzi wote kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha wanatenga maeneo mahsusi kwa ajili ya ujenzi wa masoko. Nampongeza Mheshimiwa Mbunge na Halmashauri hii ya Masasi Vijijini kwa kutenga eneo hilo, namwelekeza Mkurugenzi kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI aanze kutenga fedha kwa mapato ya ndani kwa ajili ya ujenzi wa soko hilo wakati Serikali pia ikitafuta fedha kwa ajili ya kuunga mkono juhudi hizo. Ahsante.