Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 4 Union Affairs Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 42 2024-04-05

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI aliuliza: -

Je, kuna ukweli kwamba kina cha maji ya Bahari ya Hindi hapa Tanzania kimeongezeka kutokana na mabadiliko ya tabianchi na nini athari zake?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Profesa Patrick Alois Ndakidemi, Mbunge wa Moshi Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba ni kweli kina cha maji ya Bahari ya Hindi hapa Tanzania kimeongezeka kutokana na kuendelea kuongezeka kwa joto la dunia linalosababisha kuendelea kuyeyuka kwa barafu katika maeno mbalimbali duniani. Kwa mujibu wa utafiti na vipimo vilivyopo maji ya Bahari ya Hindi katika Pwani ya Dar es Salaam yanaongezeka kwa wastani wa kiasi cha milimita sita kwa mwaka tangu mwaka 2002.

Mheshimiwa Spika, athari za kuongezeka kwa kiwango cha maji ya bahari ni pamoja na:-

(i) Kuongezeka kwa mmomonyoko na upotevu za fukwe;

(ii) Uharibifu wa miundombinu kama vile gati za bahari, barabara, nyumba ofisi na masoko;

(iii) Upotevu wa bioanuwai muhimu ikiwemo mikoko na nyasi za bahari;

(iv) Upotevu wa ardhi ya kilimo, makazi na visima vya maji baridi kuingiwa na chumvi na mafuriko ya mara kwa mara. Ahsante.