Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 43 Industries and Trade Wizara ya Viwanda na Biashara 556 2024-06-07

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha viwanda vya uzalishaji wa vyakula vya mifugo nchini?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, Serikali imeendelea kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji na kuhamasisha ujenzi wa viwanda nchini vikiwemo viwanda vya vyakula vya mifugo ambavyo vingi vinatumia malighafi za kilimo kama vile mahindi, soya na mashudu ya alizeti.

Mheshimiwa Naibu Spika, uzalishaji wa vyakula vya mifugo vilivyosindikwa umeongezeka kutoka tani 1,380,000 mwaka 2021/2022 hadi tani 1,580,000 mwaka 2022/2023. Aidha, viwanda vipya 22 vya kuzalisha vyakula vya mifugo vimesajiliwa katika mikoa nane kwa maana ya Arusha vinne, Kilimanjaro vitatu, Dar es Salaam vinne, Morogoro viwili, Iringa vitatu, Mbeya kimoja, Pwani vitatu na Shinyanga viwili na hivyo kufanya viwanda vya kuzalisha vyakula vya mifugo kuongezeka kutoka 199 mwaka 2021/2022 hadi 221 mwaka 2022/2023.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kuhamasisha uwekezaji katika viwanda vya uzalishaji wa vyakula vya mifugo na kuhakikisha kuwa vyakula vinavyozalishwa vinakuwa na viwango stahiki kulingana na mahitaji ya mifugo husika.