Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha viwanda vya uzalishaji wa vyakula vya mifugo nchini?

Supplementary Question 1

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja dogo la nyongeza lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

(a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuruhusu vyakula kutoka nje kuingizwa ndani ya nchi?

(b) Kwa kuwa chakula cha mifugo ni ghali sana jambo ambalo limekuwa ni changamoto sana kwa wafugaji; je, Serikali ina mpango gani wa kupunguza kodi kwa uingizaji wa vyakula hivyo ikiwa pamoja na kupunguza tozo? Ahsante. (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana, kwanza, nimpongeze sana Mheshimiwa Msongozi kwa ufuatiliaji kuhusiana na sekta hii ya mifugo hasa vyakula vya mifugo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa tumekuwa na changamoto ya vyakula vya mifugo vinavyozalishwa kwa maana ya kusindikwa hapa nchini ukiacha vile vya kawaida kwa maana ya nyasi na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba tuna nakisi kubwa ya uzalishaji wa vyakula vya mifugo katika viwanda vyetu na hasa katika maeneo mengine. Ni 55% tu ya vyakula vingi vinavyozalishwa kwenye sekta hii katika kulisha mifugo kwa maana ya kuku, lakini maeneo mengine bado tuna changamoto hiyo.

Kwa hiyo, mpaka sasa tayari Serikali inaruhusu vyakula vingi vilivyosindikwa kwa ajili ya mifugo vinaagizwa kutoka nje. Kwa hiyo, tunaendelea kufanya hivyo, lakini jitihada ni kuona tunazalisha sisi wenyewe ndani. Kwa hiyo, tayari hilo tunalifanya, kwa sababu tuna nakisi hiyo ya vyakula vya mifugo vinavyosindikwa katika viwanda vyetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na la pili, ni kweli tuna haja na tunaendelea kutoa vivutio vya kikodi na visivyo vya kikodi kwenye viwanda vinavyozalisha vyakula vya mifugo kwa sababu kama nilivyosema asilimia zaidi ya 60 tunaagiza kutoka nje.

Kwa hiyo, Serikali tunaendelea kuweka mipango Madhubuti ya kusaidia viwanda vya ndani na kutoa vivutio zaidi kwa wale wanaoingiza kwa sasa, lakini pia kwa wale wanaozalisha kwenye viwanda vyetu vya ndani, kwa sababu ndio haja kubwa kuona vyakula hivi vinasindikwa katika nchi yetu. Nakushukuru sana. (Makofi)