Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 43 Water and Irrigation Wizara ya Maji 557 2024-06-07

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza:-

Je, ni lini ujenzi wa Mradi wa Maji wa Miji 28 utaanza kutekelezwa katika Wilaya ya Rorya?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea na utekelezaji wa Mradi wa Maji wa Rorya - Tarime kwa kutumia chanzo cha maji ya Ziwa Victoria. Kazi zinazotekelezwa katika mradi huo ni pamoja na ujenzi wa dakio (intake) yenye uwezo wa kuzalisha maji lita milioni 29 kwa siku, ujenzi wa miundombinu ya kutibu maji (water treatment plant) yenye uwezo wa kutibu maji lita milioni 28 kwa siku, ulazaji wa mabomba umbali wa kilometa 110, ujenzi wa kituo cha kusukuma maji (booster station) pamoja na ujenzi wa matanki matatu yenye jumla ya ujazo wa lita milioni 10.

Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji wa mradi huo umefikia wastani wa 12.5% na unatarajiwa kukamilika mwezi Julai, 2025 na utanufaisha wakazi wapatao 460,885 waishio kwenye Wilaya za Rorya, Tarime pamoja na Mji wa Sirari.