Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa Mradi wa Maji wa Miji 28 utaanza kutekelezwa katika Wilaya ya Rorya?

Supplementary Question 1

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa, kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, mradi huu ndio kwanza, upo 12.5% kwa maana yake upo nyuma kulingana na muda wa kimkataba mpaka sasa na sisi wananchi wa Rorya huu ndio mradi ambao ni suluhisho kwetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nipate commitment ya Serikali, ni lini sasa Mheshimiwa Waziri mradi huu utakamilika na kuanza kutoa maji Halmashauri ya Wilaya ya Rorya?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, Mradi wa Bukura, Gabimori, Sakawa pamoja na Nyihara ni miradi ambayo imesimama kwa muda mrefu. Ninataka nijue, Mheshimiwa Waziri na imesimama, kwa sababu ya changamoto ya kifedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini fedha zitakwenda kwa ajili ya uendelezaji na ukamilifu wa miradi hiyo? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jafari Chege, Mbunge wa Rorya, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimejibu katika jibu langu la msingi mradi huu utakamilika Julai, 2025 na mpaka sasa tuna takribani miezi 12 ambayo imebaki. Namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwa sababu najua kwamba mradi huu ni wa kimkakati katika eneo lake na kwa kisiasa na kwa afya ya wananchi wake. Tunamhakikishia kwamba pesa zitaendelea kupelekwa ili mradi huu uweze kukamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa swali la pili, maeneo ya Bukura, Sakawa, Nyihara ambapo najua Nyihara ndio Mheshimiwa Mbunge anapotoka, tunatambua kwamba miradi hii inaenda kutekelezwa katika mwaka huu wa fedha. Kwa hiyo, tumwombe Mheshimiwa Mbunge atupatie ushirikiano na wananchi wake kipindi ambacho tutaanza utekelezaji ambapo ni baada ya mwezi Julai, maana yake kwamba sasa wananchi wataendelea kupata huduma ya maji safi na salama, ahsante sana. (Makofi)

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa Mradi wa Maji wa Miji 28 utaanza kutekelezwa katika Wilaya ya Rorya?

Supplementary Question 2

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Naibu Spika, je, ni lini sasa Serikali au mna mkakati gani wa kubadilisha mabomba ya zamani kuweka mapya katika Jimbo la Temeke, kwa sababu mabomba haya yanapopasuka kunakuwa na upotevu mkubwa wa maji, lakini pia uharibifu wa nyumba za watu katika eneo ambalo mabomba hayo yamepasuka? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa mabomba chakavu yanatusababishia Serikali upotevu wa maji. Tunapozalisha maji kwa mfano lita 1,000,000 na unakuta kwamba upotevu ni 40% maana yake kwamba ile production cost inaishia kwenye gharama ambazo anapelekewa mwananchi wakati maji yanayofika yanakuwa hayatoshi. Kwa hiyo, Serikali ina mkakati wa kuhakisha kwamba tunaendelea kupitia miundombinu yetu ambayo tayari imeshakuwa chakavu ili kuhakikisha kwamba tumeendelea kuibadilisha kwa kadiri fedha ambavyo tunakuwa tunapata ili kuhakikisha kwamba, upotevu wa maji angalau tunaendana na upotevu unaokubalika Kimataifa ambayo ni 15%.

Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, tutalifanyia kazi katika maeneo ya Temeke kuhakikisha kwamba wananchi wa Temeke hawapati changamoto ya maji kusambaa mitaani na wanapata maji ya uhakika ambayo ni toshelezi, ahsante sana. (Makofi)

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa Mradi wa Maji wa Miji 28 utaanza kutekelezwa katika Wilaya ya Rorya?

Supplementary Question 3

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, nikushukuru Naibu Waziri kwa ziara ya kibabe uliyoifanya katika Jimbo la Kilolo. (Makofi)

Sasa swali langu la nyongeza Mradi wa Maji wa Masege, Masalali na Kihesa Mgagao umeanza kusua sua kutokana na mkandarasi kutokulipwa kwa wakati; je, ni lini Serikali itamlipa mkandarasi ili mradi ule uweze kukamilika? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Mbunge kwa kazi nzuri anayoifanya na kwa kuendelea kushirikiana na Serikali ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na kwa kuendelea kutupatia ushirikiano na sisi tunajiona kwamba tuna mwakilishi wa wananchi ambaye anahitaji kuwasemea wananchi wake. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakuhakikishia Mheshimiwa Mbunge katika mradi huo ambao kama ambavyo umedai unasuasua Serikali kupitia Wizara ya Maji tumekaa na wenzetu Wizara ya Fedha kuhakikisha kwamba, sasa wakandarasi wetu ambao wanatekeleza mradi huo walipwe pesa ili wahakikishe kwamba mradi huo unakamilika kwa wakati na wananchi wapate huduma ya maji safi na salama, ahsante sana. (Makofi)

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa Mradi wa Maji wa Miji 28 utaanza kutekelezwa katika Wilaya ya Rorya?

Supplementary Question 4

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa nafasi; Mheshimiwa Naibu Waziri upatikanaji wa maji Mamlaka ya Mji Mdogo Namanyere ni 52% na upotevu wa maji ni 47%, tunahitaji shilingi milioni 400 tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini watatupatia hizo fedha tuweze kukarabati miundombinu iliyoharibika?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwia Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Aida, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni swali ambalo tayari Serikali tulilijibu hapa Bungeni na tayari Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Jumaa Hamidu Aweso alielekeza fedha shilingi milioni 400 zipelekwe kwa ajili ya kuhakikisha kwamba, mradi huu unakamilika. Mradi huo unapokamilika wananchi wa Namanyere wanapata huduma ya maji safi na salama, lakini vilevile unaenda kusaidia kuhakikisha kwamba, miundombinu yetu inaboreshwa na kuepusha upotevu wa maji ambao ni hasara kubwa kwa Serikali.

Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge, tuendelee kushirikiana na tutahakikisha kwamba, fedha hizo zinafika kwa wakati na mradi uendelee kutekelezwa. Tunakupongeza kwa kuendelea kufanya kazi vizuri na Serikali ya Chama Cha Mapinduzi na utekelezaji wa Ilani ya CCM inaendelea kutekelezwa vizuri sana, ahsante sana. (Makofi)