Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 43 Water and Irrigation Wizara ya Maji 558 2024-06-07

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza: -
Je, ni lini wananchi wa Kijiji cha Mtila Kata ya Matola Njombe Mjini watapelekewa maji?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuboresha huduma ya maji katika Kijiji cha Mtila Kata ya Matola Njombe Mjini, Serikali katika mwaka wa fedha 2024/2025 imetenga fedha kwa ajili ya kufanya utafiti wa maji chini ya ardhi pamoja na kuchimba kisima kirefu ili kupata chanzo cha maji. Aidha, baada ya kupatikana kwa chanzo hicho cha maji Serikali itafanya usanifu wa miundombinu ya usambazaji maji kwa ajili ya kunufaisha wananchi wa Kijiji cha Mtila, ahsante.