Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza: - Je, ni lini wananchi wa Kijiji cha Mtila Kata ya Matola Njombe Mjini watapelekewa maji?

Supplementary Question 1

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri kuhusiana na suala la Mtila nawatakia heri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza yanayohusiana na mradi mwingine wa Igongwi. Mradi muhimu sana wa kimkakati.

Swali la kwanza, mradi huu ambao utapeleka maji kwenye kata tatu na vijiji zaidi ya nane umekuwa ukisuasua, lakini tunajua umefikia 80% na kilichosababisha usikamilike kwa miaka saba ni fedha kutolewa kidogo kidogo. Swali, Serikali haioni sasa ni muda mwafaka wa kutoa fedha zote ili angalau hii 20% iliyobakia ikamilike? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, mradi huu hata fedha zote zikitolewa unaweza usikamilike kwa sababu maji yanatoka kwenye Milima ya Madope katika Wilaya ya Ludewa na yanapita Kijiji cha Luvuyo ambapo wananchi nao wanataka mradi wao ukamilike ili waruhusu maji haya yaende Njombe.

Sasa Serikali ina mkakati gani kuhakikisha maji kwenye Kijiji cha Luvuyo ambapo wananchi wamezuia yasipite wanapata fedha ili mradi wao nao ukamilike?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali kama ifuatavyo; natambua Mheshimiwa Mwanyika mradi huu kwake ni mradi wa kimkakati lakini napenda kulijulisha Bunge lako Tukufu kwamba mradi huu ni mradi wa kimkakati wa Chama Cha Mapinduzi na ni mradi wa kimkakati wa Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, tuna miradi ya kimkakati zaidi ya nane na miradi hiyo ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji, nyingine ipo katika 15%, 50% na 60% lakini kwa bahati nzuri kabisa mradi huu umeshafika katika 80% na bado 20%. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa anayoendelea kuifanya na sisi tutaendelea kuhakikisha kwamba tunaendelea kupeleka fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunapeleka fedha kulingana na upatikanaji wake kwa sababu miradi hii yote mikubwa inahitaji fedha nyingi sana na tunatamani sana Watanzania wote katika miradi hii ambayo tunaitekeleza, yote iweze kukamilika waweze kupata huduma ya maji safi na salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tutaendelea kupeleka fedha kulingana na namna ambavyo mkandarasi atakuwa analeta hati za madai.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali la pili naomba nilipokee kwa ajili ya kuwaelekeza wataalamu ili wakafanye tathmini na kujiridhisha kwamba kijiji hicho kitapata maji kutoka kwenye chanzo kipi na tukishajiridhisha basi nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tutaweza kupeleka fedha kama ambavyo ameomba kwa sababu yeye ndiyo msemaji, yeye ndiye mwakilishi wa Mheshimiwa Rais katika jimbo lake, sisi tutahakikisha kwamba tunamuunga mkono kwa kuhakikisha tunapeleka pesa kulingana na tathmini ambayo itakuwa imefanywa na wataalamu wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza: - Je, ni lini wananchi wa Kijiji cha Mtila Kata ya Matola Njombe Mjini watapelekewa maji?

Supplementary Question 2

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kuna ahadi ya muda mrefu ya kupeleka maji katika Kata ya Mnazi katika Vijiji vya Langoni A, Langoni B, Kwemkwazu pamoja na Kiwanja. Ni lini Serikali itakamilisha usanifu na ujenzi wa mradi huu wa maji katika kata hii ya kimkakati kabisa? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza kama ifuatavyo, Mheshimiwa Shangazi huu mradi na hasa Kata ya Mnazi natambua kabisa kwamba Serikali kupitia Wizara ya Maji tuna ahadi ya kufika katika kata hii. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tutafika katika kata hii na kuhakikisha kwamba tunasukuma.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo tayari Serikali imeshapata mtaalamu mshauri na gharama ya mradi ya takribani shilingi milioni 800 na tayari mtaalamu mshauri huyu ameshakabidhiwa site kwa ajili ya kuanza kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge mtaalamu wetu atakapokamilika basi tunaamini kwamba mkandarasi atapatikana kwa ajili ya kuhakikisha kwamba mradi huu unatekelezwa kwa haraka iwezekanavyo, ahsante sana.