Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 43 Energy and Minerals Wizara ya Madini 563 2024-06-07

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO K.n.y. MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: -

Je, nini mpango wa Serikali kuhakikisha uchimbaji wa Mbunyu unatekelezwa katika Kata ya Chiwata - Ndanda? (Makofi)

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Madini ilitoa leseni mbili za uchimbaji wa kati zenye namba ML 591/2018 na ML 592/2018 kwa Kampuni ya Volt Graphite Tanzania Public Limited ili kuendesha shughuli za uchimbaji wa madini ya kinywe (graphite) katika Mradi wa Mbunyu katika Jimbo la Ndanda. Hata hivyo, mradi haukuanza shughuli za uchimbaji tangu kutolewa kwa leseni hizo kutokana na kuchelewa kwa makubaliano kati ya Kampuni hiyo ya Volt Graphite na wanunuzi (off-takers). (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tayari kwa sasa mwekezaji amesaini mkataba na Kampuni ya Property Matrix Limited kwa ajili ya kufanya tathmini ya ulipaji fidia kwa wananchi waliopo katika eneo la mradi. Aidha, Kampuni ya Volt Graphite ipo katika majadiliano ya mwisho na wanunuzi (off-takers) wa graphite ili kuruhusu kuanza kwa ujenzi wa kiwanda cha kuongeza thamani madini hayo, ahsante sana.