Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 15 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 199 2024-04-29

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza kujenga Mahakama Kata ya Bwawani katika Jimbo la Arumeru Magharibi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Noah Lemburis Saputu Mollel, Mbunge wa Arumeru Magharibi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kuboresha majengo ya Mahakama katika maeneo mbalimbali nchini, hususan Mahakama za Mwanzo. Kwa sasa tunazo Mahakama 960 nchi nzima, baadhi zikiwa na majengo chakavu na ya zamani, hivyo yanahitaji kufanyiwa ukarabati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Kata ya Bwawani kwa sasa wanapata huduma za Mahakama katika Mahakama ya Mwanzo ya Nduruma ambayo kwa sasa inafanya kazi kwa kutembelewa. Mahakama hii ya Nduruma ipo umbali wa kilomita 15 kutoka Bwawani na inasajili wastani wa mashauri 120 kwa mwaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo, kwa kuzingatia umuhimu, katika mwaka wa fedha 2023/2024 tunajenga Mahakama ya Mwanzo Maji ya Chai katika Jimbo la Arumeru. Aidha, ujenzi wa Mahakama ya Bwawani utazingatiwa katika mwaka wa fedha 2026/2027 kulingana na mpango wa ujenzi na ukarabati wa majengo ya Mahakama, ahsante.