Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 45 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 579 2024-06-11

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza:-

Je, kuna mpango gani wa kuweka zege kwenye barabara za mlimani Jimbo la Same Magharibi ili kuokoa gharama za kuweka vifusi mara kwa mara?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikiweka zege kwenye barabara mbalimbali kulingana na upatikanaji wa fedha ambapo katika mwaka 2023/2024 Barabara za Makanya – Suji – Mweteni, Saweni – Gavao – Bwambo na Msanga – Chome – Ikokoa zimetengewa shilingi milioni 416.35 kwa ajili ya ujenzi wa barabara za zege zenye urefu wa kilometa 1.6 kwenye maeneo korofi na kazi inaendelea kukamilishwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, katika kipindi cha kuanzia mwaka 2017/2018 hadi 2022/2023 TARURA Wilaya ya Same imefanya matengenezo ya barabara kwa kiwango cha zege kwenye Jimbo la Same Magharibi yenye urefu wa kilometa 3.55 kwenye maeneo korofi ya barabara za milimani kwa gharama ya shilingi milioni 671.16.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga fedha za matengenezo ya barabara kwa kiwango cha zege hasa ukanda wa milimani kulingana na upatikanaji wa fedha.