Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza:- Je, kuna mpango gani wa kuweka zege kwenye barabara za mlimani Jimbo la Same Magharibi ili kuokoa gharama za kuweka vifusi mara kwa mara?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. DAVID M. DAVID: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naishukuru Serikali kwa kuanzisha mpango huo wa kuweka zege kwenye barabara za milimani kwa sababu wanapoweka vifusi pindi mvua inaponyesha barabara zile zinazolewa na tunatia hasara Serikali na wananchi wanashindwa kupita, hata hivyo na maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, Barabara za Msanga – Chome – Ikokoa – Makanya – Tae – Suji na Barabara ya Kisiwani hadi Msindo zina maeneo makorofi mengi sana, je, Serikali haioni kwamba umefika wakati wa kutenga bajeti ya kutosha kusudi barabara hizi zitengenezwe kwa kiwango cha zege ili tuweze ku-save hela za Serikali zinazotokana kumwaga vifusi ambavyo vinazolewa na mvua?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ningependa kumuuliza Mheshimiwa Waziri ni lini yuko tayari kutembelea Jimbo hili na kuziona hizi Barabara za Chome, Barabara za Makanya – Tae pamoja na Kisiwani – Msindo ili aweze kuona umuhimu wa kutenga fedha za kutosha haraka iwezekanavyo?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na nianze kwanza kwa kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa anayoifanya ya kutetea wananchi wake. Kuhusiana na swali lake la kwanza ambalo ameuliza baadhi ya barabara Serikali ina mkakati gani wa kuzijenga kwa tabaka la zege na hasa kwenye maeneo korofi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya Msanga – Chome – Ikokoa katika mwaka wa fedha huu wa 2023/2024 zimetengwa shilingi milioni 267.15 kwa ajili ya kujenga meta 100 kwa kiwango cha zege kwenye eneo korofi, lakini pia kwenye eneo hatarishi la Mlima wa Chome imejengwa strip concrete ya meta 350, lakini katika mwaka wa fedha ujao 2024/2025 Serikali imetenga jumla ya shilingi milioni 74.9 kwa ajili ya kujenga kwa kiwango cha zege meta 180 kwenye eneo hatarishi la Mlima Ikokoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuhusu Barabara ya Makanya – Tae – Suji Serikali imetenga katika mwaka wa fedha 2024/2025 milioni 161.18 kwa ajili ya kujenga kwa tabaka la zege urefu wa meta 100 kwenye eneo la Mgwasi – Tae, lakini pia ujenzi wa driffs nne za meta 32 na kwenye Barabara ya Kisiwani – Msindo, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali ilitumia shilingi milioni 250 kwa ajili ya kujenga meta 500 za strip concrete. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya kuendelea kujenga kwa kiwango cha zege kwenye maeneo hatarishi, kwenye barabara zake hizi ili ziweze kupitika kipindi chote cha mwaka mzima. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali la pili la Mheshimiwa Mbunge, naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutakaa mimi na yeye tutazungumza, tutapanga ratiba vizuri nipo tayari kutembelea Jimboni kwake kuangalia miundombinu hii ya barabara ili tuweze kuona umuhimu wa kuendelea kutenga bajeti kwa ajili ya kuzikarabati na kuzijenga vizuri. (Makofi)

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza:- Je, kuna mpango gani wa kuweka zege kwenye barabara za mlimani Jimbo la Same Magharibi ili kuokoa gharama za kuweka vifusi mara kwa mara?

Supplementary Question 2

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Serikali inaendelea kufungua barabara za mitaa kwenye Makao Makuu ya Wilaya ya Nyang’hwale pale Kharumwa kwa kiwango cha udongo. Je, Serikali ina mpango gani kuziwekea mpango wa kuweka changarawe na baadaye lami hizo barabara za mitaa Kharumwa? (Makofi)

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): Mheshimiwa Mwenyekiti, dhamira ya Serikali ni kuhakikisha kwamba inaweza kuzihudumia barabara za wilaya kwa kiwango cha lami, lakini kama wote tunavyofahamu tunaanza. Kwa hiyo, tayari Serikali imeanza kuhudumia barabara hizi kwa viwango tofauti ikiwemo viwango vya changarawe, lakini mwisho wa siku hatimaye tunataka barabara zetu zote hizi za wilaya ziwe kwa kiwango cha lami ambacho kitafanya barabara ziweze kudumu kwa muda mrefu na ziweze kupitika mwaka mzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itaendelea kutenga fedha kuhakikisha kwamba inaboresha miundombinu ya barabara zetu hizi za wilaya na hususan pia kwenye Jimbo lako Mheshimiwa Mbunge. (Makofi)

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza:- Je, kuna mpango gani wa kuweka zege kwenye barabara za mlimani Jimbo la Same Magharibi ili kuokoa gharama za kuweka vifusi mara kwa mara?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa mwenyekiti, changamoto za barabara za Mlimani kule Same Magharibi zinafanana sana na hali ilivyo kule kwetu Meru na nimeishalisema hapa mara nyingi. Kwa hiyo, sasa niulize Serikali inatoa tamko gani kuhusu barabara za milimani kule Arumeru Mashariki? Ahsante.

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge kwa kweli amekuwa akipambania sana suala la Ujenzi wa barabara kwa viwango vitakavyodumu hasa katika Jimbo lake ambalo lina milima. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwa sababu tayari tumeshazungumza na suala tayari lipo kwenye michakato na fedha tayari zimeshatengwa, nikuhakikishie Serikali itakuja kujenga barabara, itatenga fedha kila mwaka kuhakikisha kwamba inaboresha miundombinu ya barabara hizi na hasa katika jimbo lako ambalo ni la milima. (Makofi)

Name

Katani Ahmadi Katani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tandahimba

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza:- Je, kuna mpango gani wa kuweka zege kwenye barabara za mlimani Jimbo la Same Magharibi ili kuokoa gharama za kuweka vifusi mara kwa mara?

Supplementary Question 4

MHE. KATANI A. KATANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya kutoka Luagara kwenda Liponde kilometa 1.5 ilishafanyiwa feasibility study na watu wa TARURA na walishaweka kwenye bajeti miaka miwili nyuma, ni lini sasa Serikali itakwenda kuweka lami kipande kile?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu barabara hii tayari imeshafanyiwa usanifu na tayari ipo kwenye bajeti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, tutafuatilia kwa karibu hata baada ya kutoka kwenye maswali hapa tutakaa tutafuatilia kwa karibu ili tuhakikishe kwamba mwaka huu kwa sababu fedha tayari imeishatengwa ili iweze kujengwa barabara hii.