Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 45 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 580 2024-06-11

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI K.n.y. MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Shule ya Wasichana Arusha ambayo ilipangwa kujengwa katika Kata ya Enkikret – Longido?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia mradi wa kuboresha elimu ya sekondari ilipanga kujenga shule 26 za bweni za wasichana za kitaifa katika mikoa yote nchini. Lengo la shule hizi ni kuongeza fursa kwa wanafunzi wa kike kusoma masomo ya sayansi na kuwaepusha na vishawishi vinavyosababisha kukatisha masomo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa shule hizi umefanyika katika mikoa yote kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza ilianza kwa mikoa ya Kagera, Shinyanga, Mwanza, Singida, Pwani, Songwe, Lindi, Dar es Salaam, Njombe na Ruvuma. Aidha, awamu ya pili imefanyika katika mikoa iliyobaki na kufanya mikoa yote kuwa imepokea fedha za ujenzi wa shule za bweni za wasichana za mikoa ikiwemo Mkoa wa Arusha ambapo ujenzi unafanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Longido na umefikia 85%. (Makofi)