Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Emmanuel Lekishon Shangai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Primary Question

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI K.n.y. MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Shule ya Wasichana Arusha ambayo ilipangwa kujengwa katika Kata ya Enkikret – Longido?

Supplementary Question 1

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, okay kwa kuwa sasa ujenzi wa shule umefikia 85%, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ujenzi huo pamoja na nyumba za watumishi? Ahsante. (Makofi)

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze Mbunge kwa swali hili zuri sana kwa maslahi ya watoto wote wa kike ambao watasoma kwenye shule hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla ya mwaka huu wa fedha kuisha mwaka 2023/2024 Serikali itapeleka shilingi bilioni 1.1 katika shule zote zile 16 za wasichana ambazo zilipelekewa shilingi bilioni tatu awamu ya kwanza kwa ajili ya kukamilisha miundombinu ya msingi ikiwemo vyumba vya madarasa kumi, lakini chumba cha TEHAMA kimoja, maktaba moja, nyumba za walimu tatu na mabweni manne.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itapeleka fedha hii kwa ajili ya kukamilisha miundombinu ili shule zetu hizi ziweze kuwa zimekamilika na wanafunzi waweze kuingia na kuanza kuzitumia.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI K.n.y. MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Shule ya Wasichana Arusha ambayo ilipangwa kujengwa katika Kata ya Enkikret – Longido?

Supplementary Question 2

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana naomba unipe fursa nimpongeze sana Rais wa Nchi Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuliona hili kwa ajili ya wasichana. (Makofi)

Naomba kuuliza swali je, katika shule hizo zinazoenda kujengwa ambazo ni za sayansi, wamezingatia kutupatia lab technicians? (Makofi)

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): Mheshimiwa Mwenyekiti, katika ujenzi wa hizi shule kama nilivyotangulia kusema awali ukiacha majengo tu ya madarasa, lakini kutakuwa kuna chumba cha TEHAMA, kutakuwa na maktaba, nyumba za walimu na mabweni. Kwa hiyo, chumba cha TEHAMA kitakuwepo na kwa sababu msingi ni kuhakikisha kwamba shule hizi zinatoa elimu iliyobora kwa watoto wa kike, wakati wa kutoa watumishi yaani wakati wa kuajiri na kupanga watumishi kwa ajili ya kuhudumia shule hizi lazima Serikali tutazingatia ili hiki chumba cha TEHAMA kipate matumizi kiwe kina lab technicians.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI K.n.y. MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Shule ya Wasichana Arusha ambayo ilipangwa kujengwa katika Kata ya Enkikret – Longido?

Supplementary Question 3

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Wilaya ya Rungwe tuna shule nzuri sana ya wavulana. Tunashukuru Serikali kwa kuikarabati ni lini mtatujengea shule ya wasichana katika wilaya hiyo?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyotangulia kujibu kwenye majibu yangu ya msingi shule hizi zipo 26 ziko kwenye Mradi wa SEQUIP na kila mkoa inapata shule moja ya wasichana, ya bweni na ni ya sayansi. Kwa hiyo, Mkoa wa Mbeya tayari una shule moja kwa hiyo hatutojenga katika kila kata, ni shule maalum Mheshimiwa Rais amehakikisha ametenga fedha kwa ajili ya kuhakikisha kila mkoa unapata shule hii ya bweni ya wasichana ya sayansi. (Makofi)

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI K.n.y. MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Shule ya Wasichana Arusha ambayo ilipangwa kujengwa katika Kata ya Enkikret – Longido?

Supplementary Question 4

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuliona hili na kujenga na kutupatia hizo shule 26 katika nchi yetu ya Tanzania na mkoani kwetu Lindi hasa kwenye Jimbo langu kuwa ni miongoni mwa zile shule za kwanza ambazo zimejengwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, watoto wa kike wanahitaji ulinzi, je, ni lini mtatupatia pesa kwa ajili ya uzio kwa ajili kuwalinda watoto hawa? (Makofi)

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa sababu amekuwa akitetea sana, sana, sana maslahi ya watoto wa kike kupata elimu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake kama nilivyotangulia kujibu katika swali la nyongeza hapo awali Serikali italeta na itapeleka shilingi bilioni 1.1 kabla ya mwisho wa mwaka huu wa fedha kuisha, mwaka wa fedha 2023/2024 kwa ajili ya kukamilisha miundombinu yote ya msingi katika shule hizo ambazo zilipewa fedha katika awamu ya kwanza, kwa sasbabu shule hizi 16 ikiwemo shule ambayo imejengwa Mkoa wa Lindi zilipokea shilingi bilioni tatu awamu ya kwanza na sasa zitapokea mwaka huu shilingi bilioni 1.1 awamu ya pili kwa ajili ya ukamilishaji wa miundombinu yote ya msingi.