Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 45 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 581 2024-06-11

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: -

Je, ni mikataba mingapi ya mazingira na mabadiliko ya tabianchi ambayo watumishi wake wanatoka Zanzibar?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira imeridhia mikataba 12 ya kimataifa na kikanda kuhusu hifadhi na usimamizi wa mazingira na mabadiliko ya tabianchi. Utekelezaji wa mikataba hii hufanyika kwa ushirikiano na uratibu baina ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira - Tanzania Bara pamoja na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Tanzania - Zanzibar. Hivyo, utekelezaji wa mikataba hii hujumuisha watumishi wote wa pande zote mbili za Muungano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ofisi zetu mbili zimekuwa zikishirikiana kwa pamoja kwenye vikao vya maamuzi vya mikataba hii. Pia pande zote mbili za Muungano zinanufaika na utekelezaji wa mikataba hii hususani kupitia, programu na miradi inayoratibiwa kupitia mikataba hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itaendelea kusimamia utekelezaji wa mikataba ya mazingira na mabadiliko ya tabianchi kwa maslahi mapana ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kukabiliana na changamoto za kimazingira na athari za mabadiliko ya tabianchi, nakushukuru. (Makofi)