Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: - Je, ni mikataba mingapi ya mazingira na mabadiliko ya tabianchi ambayo watumishi wake wanatoka Zanzibar?

Supplementary Question 1

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, pamoja na majibu mazuri ya Serikali ninampongeza sana Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri na nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali haioni haja ya kuwa na Mratibu Msaidizi kutoka Zanzibar ili kuongeza ufanisi wa utekelezaji wa miradi hiyo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha miradi ya mazingira inamalizwa kwa wakati ili iwanufaishe walengwa? (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Maryam Azan Mwinyi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue fursa hii nimpongeze sana Mheshimiwa Maryam kutoka Mkoa wa Kusini Pemba kwa kazi nzuri anayoifanya hasa kwenye suala la mazingira na athari kubwa ya mabadiliko ya tabianchi hasa katika Mkoa wa Kusini Pemba. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar tunafanya kazi zetu kwa kushirikiana, lakini Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais - Zanzibar kwenye jambo la mazingira tunafanya kazi kwa kushirikiana. Sasa jambo la kutafuta mratibu ambaye atakuwa anasimamia haya mambo kwa sababu mambo mengi tumekuwa tunafanya kama taasisi, Wizara na Wizara, hatufanyi kama mratibu na mratibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa wazo lake na fikra yake aliyoipendekeza tunaichukua, tutakwenda kufanyia kazi kwa sababu hata wakati tunakwenda kusaini mikataba ya adaptation fund, hatukwenda kama mratibu na mratibu, tulikwenda kama taasisi na pande zote mbili tulishiriki. Tunakwenda kusaini mikataba ya EBA, tulikwenda kusaini mikataba ya miradi mbalimbali tulikwenda kama Wizara kutoka pande zote mbili. Lakini jambo la kutafuta mratibu atakayekuwa msaidizi tunalichukua na tunakwenda kulifanyia kazi. (Makofi)

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: - Je, ni mikataba mingapi ya mazingira na mabadiliko ya tabianchi ambayo watumishi wake wanatoka Zanzibar?

Supplementary Question 2

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kutokana na mabadiliko ya tabianchi kumekuwa na mafuriko makubwa katika Mto Mara ambayo yamesababisha uharibifu wa mashamba katika Vijiji vya Nyiboko, Korenga, Nyasulumunti na Iselesele, Wilayani Serengeti, je, ni lini sasa Serikali itatekeleza mradi wake mkubwa uliopangwa wa kudhibiti mafuriko hayo? Ahsante. (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Mheshimiwa aliwahi kuuliza swali hili na tuliona namna ambavyo tunaweza tukamsaidia na bahati nzuri tumeona athari kubwa ambayo inajitokeza huko na namna ambavyo wananchi wanaathirika kutokana na athari hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tumemsikia na bado Serikali tunaendelea kutafuta fedha za kuona namna ambavyo tunaweza tukatengeneza mradi huu na kuweza kuwasaidia wananchi, ili wasiendelee kusumbuka na changamoto hiyo, nakushukuru. (Makofi)