Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 18 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 231 2024-05-03

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:-

Je, lini Serikali itakamilisha zoezi la kupeleka umeme katika Shule zote na Taasisi za Dini katika Mkoa wa Kigoma?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Kigoma una vijiji 307 ambapo vijiji 257 vimepatiwa umeme na kazi ya kupeleka umeme katika vijiji 50 vilivyosalia inaendelea kupitia Mkandarasi aitwaye State Grid Electrical and Technical Works Limited anayetekeleza Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini, Awamu ya Tatu, Mzunguko wa Pili. Wakati wa uunganishaji wa wateja katika miradi, wakala hutoa kipaumbele kwa taasisi za umma zikiwemo shule na taasisi za dini. Serikali kupitia Wakala, inaendelea kuratibu upatikanaji wa umeme katika taasisi za umma vijijini, hususan Shule na Taasisi za Dini kulingana na upatikanaji wa fedha.