Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha zoezi la kupeleka umeme katika Shule zote na Taasisi za Dini katika Mkoa wa Kigoma?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, zipo shule za sekondari ambazo bado hazijapata umeme. Pamoja na shule hizo, mwaka jana, 2023 niliomba Shule ya Sekondari Kimenyi ipatiwe umeme, lakini mpaka sasa shule hiyo iliyopo Kata ya Kagera Nkanda haijaweza kupatiwa umeme. Ni lini sasa sekondari hiyo ya Kimenye itapelekewa umeme? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili. Mkoa wa Kigoma una wilaya saba. Kati ya wilaya hizo, ni wilaya nne tu ambazo zimepatiwa umeme wa gridi ya Taifa. Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika wilaya zilizosalia kwa maana ya Kigoma Vijijini, Kigoma Mjini na Uvinza? (Makofi)

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na kupeleka umeme katika Shule ya Kimenyi iliyopo katika Kijiji cha Kagera Nkanda, tayari mkandarasi ambaye anatekeleza mradi wa kupeleka umeme katika Kijiji cha Kagera Nkanda yupo site. Sasa nimwelekeze Meneja wa Mkoa wa Kigoma ahakikishe anatenga fungu la ziada kwa sababu shule hii ipo mita 900 kutoka kwenye njia ya umeme anayojenga mkandarasi. Kwa hiyo, pale ambapo njia hii itakamilika, basi watenge fungu la nyongeza kwa ajili ya kuunganisha umeme kwenda kwenye shule hii ya sekondari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na kupeleka umeme wa gridi katika hizi wilaya tatu, Serikali inatekeleza mradi wa kupeleka umeme wa gridi katika Mkoa wa Kigoma ambapo mradi huu kwa sasa umefikia asilimia 94. Namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kuwa mradi unaendelea vizuri sana na tunajenga njia ya umeme ya kilovoti 400 kutoka Nyakanazi hadi Kidahwe. Umeme ukifika Kidahwe utaenda Kigoma Mjini pamoja na Uvinza kwa kadiri ya utekelezaji wa mradi ambao upo kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwahakikishie wananchi wa Kigoma kuwa mradi wa kupeleka gridi ya umeme Kigoma unaendelea vizuri sana na utamalizika kwa wakati. (Makofi)

Name

Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha zoezi la kupeleka umeme katika Shule zote na Taasisi za Dini katika Mkoa wa Kigoma?

Supplementary Question 2

MHE. MAIMUNA A. PATHAN: Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni lini Serikali itakamilisha zoezi la kupeleka umeme katika shule na taasisi zote zikiwepo za dini katika Mkoa wa Lindi?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika miradi ambayo inaendelea, ni maelekezo ya Serikali kwamba shule na taasisi ambazo zipo mita chache katika maeneo ambayo tunapitisha njia za umeme, basi taasisi hizi ziweze kuunganishwa. Zile ambazo zipo umbali wa zaidi ya mita 900 kwenda nyuma, ni maelekezo kwamba Ofisi zetu za Mikoa na Ofisi za TANESCO za kimkoa zihakikishe zinatenga bajeti ya ziada na nyongeza kuhakikisha zinapeleka umeme katika taasisi hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni maelekezo ya Serikali kuhakikisha taasisi zote za msingi zinapata umeme kwa ajili ya ustawi wa watu wetu na shughuli za maendeleo za wanajamii.

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha zoezi la kupeleka umeme katika Shule zote na Taasisi za Dini katika Mkoa wa Kigoma?

Supplementary Question 3

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni lini umeme unaopita eneo la Uhasibu utakamilika ili Jimbo la Temeke tuweze kupata umeme usiokatikakatika tena?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la Kurasini ni kweli limekuwa lina changamoto ya umeme, lakini tuna ujenzi wa laini ya chini ya umeme kwa ajili ya kuboresha umeme katika Wilaya ya Ilala. Namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba mradi unaendelea vizuri sana na upo katika hatua za mwisho za umaliziaji. Pindi utakapokamilika, wananchi wa jimbo lako watapata umeme wa uhakika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuhakikishia tunasimamia mradi huu kwa weledi mkubwa sana kuhakikisha unakamilika kwa wakati.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha zoezi la kupeleka umeme katika Shule zote na Taasisi za Dini katika Mkoa wa Kigoma?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni lini Serikali itapeleka umeme kwenye vijiji vilivyobakia kwenye Wilaya ya Kilosa pamoja na Morogoro Vijijini? Ahsante sana.

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI:Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Wilaya ya Kilosa na Morogoro Vijijini wakandarasi wapo site. Tunaendelea kuwahimiza wakandarasi kutekeleza miradi hii kwa weledi kuhakikisha wananchi wanapata umeme kwa wakati na kuhakikisha wanakamilisha majukumu yao kulingana na mikataba yao, ahsante.

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha zoezi la kupeleka umeme katika Shule zote na Taasisi za Dini katika Mkoa wa Kigoma?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Jimbo la Muleba Kusini ina vijiji vitatu ambavyo havijapata umeme; Kijiji cha Kiholele, Burungura na Bihanga. Ni lini Serikali itapeleka umeme katika vijiji hivyo?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hivi vijiji vitatu kwenye Jimbo la Mheshimiwa Dkt. Kikoyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mkandarasi yupo site. Tutaendelea kumsimamia ili aongeze kasi kuhakikisha vijiji hivi vinawaka umeme.