Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 18 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 233 2024-05-03

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:-

Je, kuna utafiti wa kisayansi unaoonyesha kufunga shughuli za uvuvi Ziwa Tanganyika kuruhusu kuzaliana kwa Samaki kutakuwa na tija?

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuhakikisha uvunaji wa rasilimali za uvuvi katika Ziwa Tanganyika unafanyika kwa njia endelevu, Wizara kwa kushirikiana na nchi zinazounda Mamlaka ya Ziwa Tanganyika inatekeleza Mkataba wa Kikanda wa Nchi Wanachama wa Mamlaka ya Ziwa Tanganyika unaoweka hatua za usimamizi wa uvuvi endelevu katika Ziwa Tanganyika na Bonde lake. Aidha, miongoni mwa hatua za usimamizi ni kuanzishwa kwa utaratibu wa kupumzisha shughuli za uvuvi katika Ziwa Tanganyika kila ifikapo tarehe 15 Mei hadi 15 Agosti ya kila mwaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, upumzishaji wa Ziwa Tanganyika katika kipindi cha miezi mitatu, unatarajiwa kuwa na tija ya muda mrefu kwa kuwa tafiti katika nchi zinazozunguka ziwa zinaonesha kuwa kipindi hicho kunakuwepo na samaki wengi wachanga aina ya migebuka na dagaa. Samaki hawa wanahitaji kipindi cha miezi mitatu mpaka minne kufikia kiwango cha kuvuliwa. Aidha, kupumzisha ziwa katika kipindi hicho kutaruhusu samaki kukua na mavuno kuongeza.