Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 18 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 236 2024-05-03

Name

Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE K.n.y. MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: -

Je, lini ujenzi wa Barabara ya Katoro hadi Ushirombo hususani kipande cha Katoro hadi Luhembero utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Katoro hadi Ushirombo yenye urefu wa kilometa 58.2 unatekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Kwa sasa maandalizi kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa sehemu ya Nyikonga hadi Kashelo kilometa 10.5 yanaendelea chini ya ufadhili wa Benki ya Dunia ambapo mkataba kwa ajili ya kuanza ujenzi unatagemewa kusainiwa mwezi Agosti, 2024. Kwa sehemu zilizobaki za Katoro – Nyikonga kilometa 26.2 na Kashelo – Ushirombo kilometa 21.5, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami, ahsante.