Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edwin Enosy Swalle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE K.n.y. MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, lini ujenzi wa Barabara ya Katoro hadi Ushirombo hususani kipande cha Katoro hadi Luhembero utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. EDWIN E. SWALLE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naishukuru sana Serikali na Wizara hii ya Ujenzi, wanafanya kazi nzuri sana nchini kwa ajili ya ujenzi wa barabara. Sasa ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza. Wananchi wa Jimbo la Lupembe nao wanahitaji barabara. Kumekuwa na ahadi ya muda mrefu ya Barabara ya Kibena – Lupembe mpaka Madeke. Ni lini barabara hii itaanza ujenzi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, mwaka 2022 tuliomba barabara ya wananchi wa Mtwango – Kichiwa kwenda Ikuna, ipandishwe hadhi kuwa barabara ya TANROADS, iweze kujengwa kwa lami. Je, ni upi mpango wa Serikali kujenga barabara hii? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikianza na swali la kwanza, barabara ya Kibena Junction - Lupembe – Madeke – Mlimba hadi Ifakara tayari tumeshaanza utekelezaji kwa kuijenga kwa kiwango cha lami. Kwa upande wa Morogoro tayari tuna kilometa 100 ambazo tumeshaanza kuzijenga na Wakandarasi wako site kwenye lot ya kwanza na nyingine tumeshasaini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa kuanzia Mkoa wa Njombe kwenye Jimbo la Mheshimiwa Swalle, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, kwanza yalikuwa ni maelekezo ya Rais na alitoa ahadi kwamba barabara hiyo ianze kujengwa kwa kiwango cha lami na tunavyoongea tuko kwenye hatua za mwisho za manunuzi tukianza na kilometa 42 kuanzia Kibena junction. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuwa mradi huo upo na tupo kwenye hatua za mwisho za manunuzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili kuhusu kupandisha hadhi kwa maana ya barabara kutoka TARURA kwenda TANROADS, nimjulishe Mheshimiwa Mbunge kwamba ziko taratibu ambazo kama Wilaya na Mkoa wakishakamilisha taratibu zote wanaleta taarifa kwa Mheshimiwa Waziri ambaye baadaye anatuma timu ambayo inaenda kufanya tathmini ya ile barabara. Kwa hiyo, kama hatua zote zimekamilika nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuwa tutakupa majibu ya kuipandisha hadhi hiyo barabara kama itakidhi vigezo, ahsante. (Makofi)

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE K.n.y. MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, lini ujenzi wa Barabara ya Katoro hadi Ushirombo hususani kipande cha Katoro hadi Luhembero utaanza?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, je, lini ahadi ya siku nyingi ya Serikali ya ujenzi wa barabara ya Kilolo – Kisinga – Wotalisoli – Mlafu hadi Ilula, itakamilika? Barabara hii ikikamilika watu watakuwa hawaendi mpaka mjini. Naomba Serikali itoe majibu ili wananchi wa Kilolo wasipate matatizo makubwa.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara aliyoitaja Mheshimiwa Dkt. Ritta Kabati amekuwa anaifuatilia sana. Nimhahakishie kwamba tayari tumeshalichukua, tulishawaelekeza wenzetu wa TANROADS na TARURA Mkoa wa Iringa waweze kutoa tathmini ya awali ili tuweze kuingiza kwenye mpango wa kuifanyia usanifu wa kina, ahsante.

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE K.n.y. MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, lini ujenzi wa Barabara ya Katoro hadi Ushirombo hususani kipande cha Katoro hadi Luhembero utaanza?

Supplementary Question 3

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Barabara ya Kasamwa kupitia Nyaseke kwenda Nyang’hwale inaunganisha Wilaya mbili, lakini sasa hivi madaraja yote yamekatika na iko chini ya TARURA ambao hawana uwezo wa kuijenga. Ni lini TANROADS wanaweza kukubali kuihamishia huko ili iweze kutengezwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge kwamba, sasa tunavyoongea TARURA imeimarika sana. Ina wataalam na hata bajeti yake imeongezeka kwa kiasi kikubwa sana. Kwa hiyo, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kama kutakuwa na changamoto ya kitaalamu TANROADS mara nyingi tumekuwa tukisaidiana na wenzetu wa TARURA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tumelipokea na hii nadhani inaenda kwa miundombinu yote ikiwa ni pamoja na madaraja yote Tanzania ambayo yameharibika iwe ya TARURA ama ya TANROADS. Hivyo, tumelipokea, namwagiza Meneja wa TANROADS, Geita waweze kuwasiliana na mwenzake wa TARURA Mkoa wa Geita waone namna watakavyoshirikiana, ahsante. (Makofi)

Name

George Natany Malima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE K.n.y. MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, lini ujenzi wa Barabara ya Katoro hadi Ushirombo hususani kipande cha Katoro hadi Luhembero utaanza?

Supplementary Question 4

MHE. GEORGE N. MALIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini ujenzi wa Daraja la Godegode linalounganisha majimbo mawili, Jimbo la Kibakwe na Jimbo la Mpwapwa utaanza? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Daraja la Godegode lilikuwa limeshapata Mkandarasi lakini alijitoa likatangazwa upya. Tunavyoongea sasa hivi, tumeshapata Mkandarasi mwingine, tuko kwenye majadiliano ya mwisho ili aweze kuanza kazi ya kulijenga hilo Daraja la Godegode, ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE K.n.y. MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, lini ujenzi wa Barabara ya Katoro hadi Ushirombo hususani kipande cha Katoro hadi Luhembero utaanza?

Supplementary Question 5

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na shukrani nyingi kutoka kwa wananchi wa Nyasa, kwa kuwa barabara ya kutoka Rwanda mpaka Ndumbi kipande hiko kimeshasainiwa tayari, je, Serikali haioni kwamba ni vema sasa ikaanza kujenga kutokea Ndumbi – Lituhi na kuelekea Rwanda badala ya utaratibu wa kutokea Rwanda kuja Ndumbi? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani hilo ni ombi na pendekezo la Mheshimiwa Mbunge. Sisi tunaomba tulipokee na tutaliangalia, kama kitaalam na kiutekelezaji litatufaa hatutokuwa na shida kwa sababu cha msingi ni kuijenga hiyo barabara yote kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo, tumelipokea Mheshimiwa Mbunge. (Makofi)