Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 18 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 239 2024-05-03

Name

Martha Nehemia Gwau

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA N. GWAU aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kufufua usafiri wa Reli kutoka Dodoma kwenda Singida?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Shirika la Reli Tanzania (TRC) ina mpango wa ufufuaji na ukarabati wa miundombinu ya Reli ya Kati yenye kiwango cha Meter Gauge. Aidha, TRC inaendelea na ukarabati na uboreshaji wa Njia Kuu kutoka Dar es Salaam - Isaka ambapo kwa awamu ya kwanza uboreshaji umefanyika kutoka Dar es Salaam hadi Tabora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa awamu ya pili, Serikali ina mpango wa kuboresha kipande cha Tabora – Isaka ikiwemo kukarabati kipande cha Dodoma – Manyoni kwa maeneo yaliyobaki wakati wa utekelezaji wa awamu ya kwanza. Vilevile, Serikali inafanya tathmini ya ukarabati wa njia ya reli ya Manyoni – Singida ili kuimarisha shughuli za kiuchumi kupitia usafiri wa reli kwa kuunganisha ukanda huo.