Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Martha Nehemia Gwau

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA N. GWAU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufufua usafiri wa Reli kutoka Dodoma kwenda Singida?

Supplementary Question 1

MHE. MARTHA N. GWAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza: Je, ni lini Serikali italipa fidia kwa wananchi waliopisha maeneo yao kwa ajili ya ujenzi wa SGR, ambao ni wananchi wa Halmashauri ya Itigi na wananchi wa Halmashauri ya Manyoni?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili: Ni lini Serikali italipa Service Levy kutokana na ujenzi wa reli ya SGR kwa hizi Halmashauri ambazo zimepitiwa na reli hii; Halmashauri ya Itigi na Halmashauri ya Manyoni? Nashukuru.

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia malipo hayo, nataka nimjulishe kwamba mfumo wa utoaji wa ardhi katika eneo hilo umekuwa ukienda sambamba na kulipa fidia. Maeneo ambayo hayajalipwa fidia kwa sasa ni yale maeneo ambayo tuna uchimbaji wa malighafi ya ujenzi ikiwa ni pamoja na Tambukareli, Centre pamoja na Milembela. Maeneo hayo yataendelea kulipwa kulingana na hatua za uthamini zitakapokamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili kuhusiana na Service Levy kwa Halmashauri zote mbili kwa maana ya Itigi pamoja na hiyo nyingine ya Manyoni, tulifanya vikao mwaka jana, 2021 kati ya TRC pamoja na Halmashauri zote mbili, namshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatiliaji wake baada ya kukubaliana ikaonekana kwamba pengine inatakiwa waanze kulipwa shilingi 1,500,000,000 kwa kila Halmashauri moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi ninavyozungumza, tayari wameshalipwa shilingi 214,000,000 kila mmoja na malipo mengine yataendelea kufanyika kulingana na jinsi tutakavyokuwa tumechimba zile material. (Makofi)