Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 18 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 241 2024-05-03

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza: -

Je, lini Kimondo cha Ivuna kitarejeshwa nchini na kutumika kama kivutio cha utalii?

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua kuwepo kwa kimondo kilichoanguka Kijiji cha Ivuna, Mkoa wa Songwe mwaka 1938 kikiwa na ujazo wa tani 0.0077 sawa na asilimia 0.0044% ya kimondo cha Mbozi kilichopo katika Kijiji cha Isele Mkoani Songwe chenye tani 16.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Kimondo cha Ivuna kinahifadhiwa kwenye Makumbusho ya Historia ya Asili iliyo katika Mji wa London Nchini Uingereza. Aidha, Wizara kwa kutambua umuhimu wa malikale zilizochukuliwa nchini kabla na baada ya uhuru kwa sababu mbalimbali kikiwemo Kimondo cha Ivuna, imeunda Kamati ya Kitaifa inayoratibu namna bora ya kurudisha au kunufaika na malikale hizo zilizopo nje ya nchi. Kamati inafuatilia taarifa zake ili kuweza kuishauri Serikali njia sahihi za kukirudisha.