Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza: - Je, lini Kimondo cha Ivuna kitarejeshwa nchini na kutumika kama kivutio cha utalii?

Supplementary Question 1

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa ni miaka 86 toka kimondo hiki kichukuliwe kule Ivuna Jimbo la Momba, kimekuwa kikihifadhiwa kwenye hiyo museum iliyopo huko London. Je, sisi kama Wana-Momba tutanufaika vipi na kile ambacho wanakipata kwenye museum yao na Taifa kwa ujumla, baada ya miaka 86?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Mahali hapo ambapo kilichukuliwa kimondo kwenye Kijiji cha Itumbula Kata ya Ivuna zipo taarifa nyingi ambazo zinazunguka eneo hilo ambazo zinavutia kwa ajili ya mambo ya utalii. Je, ni lini Wizara ya Maliasili na Utalii mtafika eneo hilo la Itumbula, Ivuna ili mweze kukutana na wazee wa mahali hapo tuweze kuwasimulia historia nzuri ya kupendeza katika eneo hilo?

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi kwamba Serikali imeunda timu ya Kitaifa ya kuishauri namna bora ya kunufaika na uwepo wa malikale katika nchi za wenzetu ambazo zimetokea katika nchi yetu. Namwomba Mheshimiwa Mbunge awe na subira, Kamati hii au timu hii inafanyia kazi mambo haya na itaishauri Serikali namna nzuri ya sisi kunufaika na malikale hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye swali lake la pili kwamba ni lini tutakwenda kwenye eneo lile, nataka kumfahamisha Mheshimiwa Mbunge kwamba Wizara tayari imeshafika kwenye eneo lile na imeanzisha tamasha ambalo hufanyika kila mwezi Juni. Tamasha hilo linaibua fursa za kiutalii kwenye eneo hilo na wataalamu wetu wanakamilisha michakato ya kujumuisha eneo hili liwe sehemu ya tamasha linalofanyika katika mkoa ule.

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza: - Je, lini Kimondo cha Ivuna kitarejeshwa nchini na kutumika kama kivutio cha utalii?

Supplementary Question 2

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa kupitia Ilani ya Chama chetu tuliwaahidi wananchi kwamba kwenye mapori yetu tutatenga maeneo ya kuishi watu, lipo pori la Kigosi ambalo limepakana na Kata ya Iponya na Kata ya Bukandwe: Ni lini Serikali itatenga maeneo ya kuishi watu ili waweze kufanya shughuli zao na kuishi kwa uhuru na amani kwenye hiyo hifadhi?

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali hili lililoulizwa ni tofauti sana na swali la msingi. Naomba kumshauri Mheshimiwa Mbunge alilete swali hili kama swali mahsusi ili niweze kulijibu kikamilifu.