Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 39 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 332 2016-06-09

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE aliuliza:-
Mwezi Septemba, 2015 Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli, aliwaahidi wananchi wa Kata za Busonzu, Busagara na Murungu ambao wamepakana na Hifadhi ya Taifa ya Muyowosi kwamba mpaka kati ya wananchi hao na hifadhi hiyo, utarekebishwa ili wananchi wapate eneo kwa ajili ya kilimo.
Je, utekelezaji wa ahadi hiyo utaanza lini?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mhandisi Atashasta Justus Nditiye, Mbunge wa Muhambwe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu kupitia uongozi wa Serikali ya Wilaya ya Kibondo inayo taarifa ya maombi kutoka kwa wananchi wa Kata za Busonzu, Busagara na Murungu kuongezewa maeneo kutoka Pori la Akiba la Moyowosi kwa matumizi ya shughuli za kibinadamu, ikiwa ni pamoja na shughuli za kiuchumi na kijamii katika vijiji vya kata hizo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu itayaorodhesha maombi haya katika orodha ya maeneo yanayopakana na hifadhi, yatakayoshughulikiwa kimkakati na Serikali; kwa kushirikisha wadau wote muhimu, zikiwemo Wizara za Maliasili na Utalii, Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, TAMISEMI, Maji, Nishati na Madini na Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, kwa nchi nzima. Utaratibu huu unaotarajiwa kuanza baada ya Mkutano wa Tatu wa Bunge la Kumi na Moja kukamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu inaendelea kusisitiza kwamba utekelezaji wa azma ya Serikali ya kujibu kero za wananchi kuhusu changamoto za mahitaji ya ardhi, utazingatia uwepo wa sheria, kanuni na taratibu na pia kuweka mbele maslahi ya Taifa. Aidha Hifadhi ya Pori la Akiba la Moyowosi lilianzishwa kisheria, kwa Tangazo la Serikali namba moja, la mwaka 1981 baada ya kukidhi vigezo vyote, ikiwemo ushirikishwaji wa wananchi katika hatua za Vijiji, Kata, Mkoa hadi Taifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, umuhimu wa kuhifadhi Pori la Akiba la Moyowosi Kitaifa, unazingatia bioanuwai katika mfumo wa ikolojia ya Moyowosi Malagarasi. Inayotoa mchango mkubwa wa viumbe mbali mbali wanaopatikana katika maeneo hayo, pamoja na utunzaji wa vyanzo vya maji kwa matumizi ya binadamu. Eneo hilli pia ni sehemu ya ardhi ya owevu, yenye hadhi ya kimataifa yaani Ramsar Site.