Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 38 Water and Irrigation Ofisi ya Rais TAMISEMI. 313 2016-06-07

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RITTA E. KABATI (K.n.y. MHE. GRACE V. TENDEGA) aliuliza:-
Katika miaka ya 1990, Wilaya ya Iringa Vijijini kulikuwa na mradi wa usambazaji wa maji kwa kutumia chanzo cha maji ya Mto Mtitu ili kuondokana na adha ya maji inayowakumba wananchi wa Iringa Vijijini; juhudi za kufanya upembuzi yakinifu zilifanyika ili kuweza kusambaza maji kwa gravity kwenye vijiji vyote vya Kata za Maguliwa, Luhota, Mseke, Ifunda, Mgama na Maboga:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha mradi huu ili kuweza kuondoa tatizo la maji kwa wananchi wa Kata hizo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Grace Victor Tendega, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Iringa kwa kushirikiana na Wizara ya Maji na Umwagiliaji, imepanga kufanya usanifu wa kina wa mradi mkubwa wa maji ambao utahusisha vijiji vya Kata za Ngawila, Luhota, Mseke, Ifunda, Mgama na Lugonga. Lengo ni kubaini uwezo wa chanzo cha Mto Mtitu katika kuhudumia maeneo hayo yote. Kazi hiyo imepangwa kufanyika katika bajeti ya mwaka wa fedha 2016/2017, ambapo zimetengwa Shilingi milioni 49.5. Mradi huo utakapokamilika, jumla ya vijiji 17 vyenye wakazi wapatao 36,397 vitanufaika.