Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RITTA E. KABATI (K.n.y. MHE. GRACE V. TENDEGA) aliuliza:- Katika miaka ya 1990, Wilaya ya Iringa Vijijini kulikuwa na mradi wa usambazaji wa maji kwa kutumia chanzo cha maji ya Mto Mtitu ili kuondokana na adha ya maji inayowakumba wananchi wa Iringa Vijijini; juhudi za kufanya upembuzi yakinifu zilifanyika ili kuweza kusambaza maji kwa gravity kwenye vijiji vyote vya Kata za Maguliwa, Luhota, Mseke, Ifunda, Mgama na Maboga:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha mradi huu ili kuweza kuondoa tatizo la maji kwa wananchi wa Kata hizo?

Supplementary Question 1

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Naomba niulize maswali mawili tu ya nyongeza. Kwa kuwa Mkoa wa Iringa hasa katika Wilaya za Kilolo, Iringa Vijijini, Isimani, Kalenga na Mufindi, miradi mingi sana ya maji imekuwa haikamiliki kwa wakati na kusababisha wanawake wengi sana hata ndoa zao zimekuwa hatiani kwa sababu ya baridi; wamekuwa wakiamka asubuhi sana kwenda kutafuta maji. Je, ni lini sasa miradi ile iliyopo katika Mkoa wetu wa Iringa, Serikali itafanya kwa uharaka zaidi, pamoja na kuponya ndoa za wanawake wa Iringa? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; Wakandarasi wengi sana wamekuwa wakikamilisha miradi, lakini Serikali imekuwa haiwalipi madai yao kwa wakati. Je, ni mkakati gani umewekwa na Serikali kuhakikisha Wakandarasi hawa wanalipwa kwa wakati ili hii miradi iweze kukamilika kwa wakati?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote naomba kutoa pole sana kwa wale ambao ndoa zao zimeingia hatiani, mashakani kwa hiyo changamoto ya maji. Naomba niwasihi akinababa kwamba hawa akinamama msiwahukumu katika hilo kwa sababu wanachokifanya ni kuwatafutia maji watoto na ninyi akinababa wenyewe.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika eneo la kwanza ni kwamba lini miradi hii itakamilika? Katika vipindi mbalimbali nimeelezea hapa, ni kweli miradi mingi ya maji imechelewa kukamilika kwa muda na watu mnafahamu ile miradi ya World Bank hasa tuliyokuwa tukiitekeleza katika kipindi kilichopita ambayo mpaka sasa tunaendelea nayo, ni kwamba miradi mingi Wakandarasi waliweza kutoa vifaa kutoka site, ni kwa sababu Wakandarasi wengi sana wali-raise certificate lakini walikuwa hawajalipwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto kubwa kama nilivyosema awali, ni kwamba, kwa sababu mwaka uliopita ulikuwa ni wenye changamoto kubwa sana, kwani fedha za miradi hazikwenda vizuri. Kama nilivyosema, katika Serikali hii ya Awamu ya Tano jukumu lake kubwa lilikuwa ni kukusanya kodi na mnafahamu kwamba tokea mwezi wa 12 mpaka hivi sasa, makusanyo ya kodi kila mwezi tumevunja rekodi ukilinganisha na kipindi kilichopita.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana certificate zote zilizokwenda katika Wizara ya Maji, zimelipwa na hata Naibu Waziri wa Maji juzi juzi hapa alikuwa anasema kwamba Mkandarasi yeyote mwenye certificate ambaye anatakiwa alipwe, afikishe haraka Wizara ya Maji pesa hizo zitalipwa. Ndiyo maana wale Wakandarasi wote waliokuwa hawajalipwa mwanzo, sasa hivi wote wamelipwa. Imani yetu kubwa ni kwamba sasa miradi hiyo itakwisha kwa sababu Wakandarasi wote wako site.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu madai yao kwamba ni lini yatalipwa? Ndicho nilichokisema hapa katika majibu yangu ya awali, kwamba sasa pesa zote za Wakandarasi wote zimeshapelekwa katika Halmashauri. Tunachohitaji ni kwamba zile certificate ambazo Wakandarasi wamelipa, Wakurugenzi wa Halmashauri wafanye haraka waweze kulipwa pesa zao ilimradi kwamba ile miradi iweze kukamilika na wananchi wetu waweze kupata huduma ya maji.

Name

Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. RITTA E. KABATI (K.n.y. MHE. GRACE V. TENDEGA) aliuliza:- Katika miaka ya 1990, Wilaya ya Iringa Vijijini kulikuwa na mradi wa usambazaji wa maji kwa kutumia chanzo cha maji ya Mto Mtitu ili kuondokana na adha ya maji inayowakumba wananchi wa Iringa Vijijini; juhudi za kufanya upembuzi yakinifu zilifanyika ili kuweza kusambaza maji kwa gravity kwenye vijiji vyote vya Kata za Maguliwa, Luhota, Mseke, Ifunda, Mgama na Maboga:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha mradi huu ili kuweza kuondoa tatizo la maji kwa wananchi wa Kata hizo?

Supplementary Question 2

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri. Swali; je, wale Wakandarasi au Halmashauri zilizolipa pesa kwa Wakandarasi hewa, mtachukua hatua gani? Kuna miradi kadhaa katika Wilaya ya Nkasi ambayo pesa zililipwa lakini hakuna kilichofanyika.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA Mheshimiwa Naibu Spika, kama Mkandarasi amelipwa lakini kazi hajafanya, maana yake huo ni wizi; jambo la kwanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwaambie na hili tumelisema katika vipindi mbalimbali, Wakandarasi wowote ambao kwa njia moja au nyingine wamechukua fedha na kazi wametelekeza, tutahakikisha, nami nitawaomba Wakurugenzi wote waweze kuwabainisha; hasa wale Wakandarasi wa maji waliotekeleza miradi katika maeneo yao. Kwa sababu tukirejea katika Bunge lililopita, Waziri wa Maji hapa alisema wazi kwamba Wakandarasi ambao watashindwa kutekeleza wajibu wao watafutiwa hata suala la kupata tenda katika nchi yetu. (Makofi)
Kwa hiyo, Mheshimiwa Keissy, naomba tukitoka hapa unipe rejea ya hao Wakandarasi ili mradi tuweze kuwafanyia kazi. Lengo kubwa ni kwamba, wananchi wetu waweze kupata huduma ya maji.

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, TAMISEMI, hoja ya Mheshimiwa Keissy ndiyo tumeshaanza kuifanyia kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Maji na Umwagiliaji tumeamua kuchukua hatua kwamba hatuwezi kupeleka hela kwenye Halmashauri mpaka walete certificate. Tumefikia hili kwa sababu hela zilikuwa zinapelekwa, halafu zinatumika, lakini ukienda kule hakuna kilichofanyika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyozungumza huko nyuma katika Bunge hili, ni kwamba tunakwenda kuunda Kamati ya Wataalam. Utaleta certificate yako kabla hatujailipa, tutatuma wataalam kwenye eneo twende tukaangalie kama hiyo kazi imefanyika ili tuweze kupambana na hili suala ambalo lilitaka kutupeleka pabaya.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. RITTA E. KABATI (K.n.y. MHE. GRACE V. TENDEGA) aliuliza:- Katika miaka ya 1990, Wilaya ya Iringa Vijijini kulikuwa na mradi wa usambazaji wa maji kwa kutumia chanzo cha maji ya Mto Mtitu ili kuondokana na adha ya maji inayowakumba wananchi wa Iringa Vijijini; juhudi za kufanya upembuzi yakinifu zilifanyika ili kuweza kusambaza maji kwa gravity kwenye vijiji vyote vya Kata za Maguliwa, Luhota, Mseke, Ifunda, Mgama na Maboga:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha mradi huu ili kuweza kuondoa tatizo la maji kwa wananchi wa Kata hizo?

Supplementary Question 3

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kufahamu, kule Jimboni Mbulu kuna Bwawa la Dongobesh lililokamilika takriban miezi sita. Mkandarasi ameshaleta certificate yapata miezi miwili. Waheshimiwa Mawaziri wanajibu majibu hapa, lakini kule Wizarani hakuna mchakato wa kuwalipa hao Wakandarasi. Naomba, kama itawezekana, Waziri ana kauli gani kumlipa Mkandarasi wa Bwawa la Dongobesh?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, Bwawa la Dongobesh ni kweli ujenzi wake umeshakamilika, kilichobaki ni miundombinu ili lile bwawa sasa liweze kufanya kazi kwenda kumwagia kwenye mashamba. Tumeweka utaratibu kwamba certificate zifike. Wiki iliyopita niliongea na Mheshimiwa Mbunge kwamba mpaka wiki iliyopita certificate zilikuwa hazijawasilishwa katika Wizara, lakini tunaendelea kufuatilia.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimeshamwagiza Mkurugenzi wa Maji Vijijini ili aweze kuwasiliana na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mbulu Vijijini ili waweze kuangalia hizi certificate ziko wapi, kwa sababu kule wanasema zimetumwa, lakini Wizarani hazijafika. Kwa hiyo, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba hili suala tunalifanyia kazi na pindi certificate zikifika hela tunazo, tunalipa, ili hili bwawa liweze kukamilishwa.