Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 36 Energy and Minerals Wizara ya Madini 297 2016-06-03

Name

Janet Zebedayo Mbene

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ileje

Primary Question

MHE. JANET Z. MBENE aliuliza:-
Ileje inatambuliwa kuwa ndiyo inayokalia ardhi inayotoa makaa ya mawe yanayoitwa Kiwira Coal Mine lakini mgodi huu haujawanufaisha wananchi wa Ileje kwa muda wote uliokuwa ukifanya kazi mpaka ulipofungwa:-
(a) Je, ni lini mwekezaji mpya ataanza uzalishaji tena kwenye mgodi?
(b) Je, ni lini tutakaa na mwekezaji huyu kama halmashauri ili kufahamiana?
(c) Je, ni lini tutapata mwekezaji wa kutumia makaa haya kuzalisha umeme?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Janet Zebedayo Mbene, Mbunge wa Ileje, lenye sehemu (a), (b) na (c) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kiwira (Kiwira Coal Mine) unamilikiwa na Serikali kwa asilimia 100 na kusimamiwa na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO). STAMICO wanamiliki leseni maalum ya uchimbaji mkubwa yenye usajili namba SML.233/2005 itakayodumu kwa miaka 25. STAMICO wanatarajia kuzalisha umeme megawati 200 kwa gharama ya Dola za Marekani milioni 500.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mwaka huu wa fedha 2015/2016, shirika liliweza kukamilisha Rasimu ya mwisho ya Upembuzi wa Mazingira kwa mradi wa Open Cast, wa kuzalisha megawati 200. Hata hivyo, mradi huo, pia unahusisha usafirishaji wa msongo wa kilovoti 400 yenye urefu wa kilometa 100 kutoka Kiwira hadi Mwakibete, Mbeya.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa STAMICO ipo katika hatua za kumtafuta mzabuni kuendeleza mgodi huo lakini taratibu za kumpata mwekezaji zinaendeleza na zinatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2016. Mara tu mwekezaji atakapopatikana, atatambulishwa kwa viongozi wa Halmashauri za Rungwe na Ileje ambazo sehemu ya mradi huu unapatikana.