Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Janet Zebedayo Mbene

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ileje

Primary Question

MHE. JANET Z. MBENE aliuliza:- Ileje inatambuliwa kuwa ndiyo inayokalia ardhi inayotoa makaa ya mawe yanayoitwa Kiwira Coal Mine lakini mgodi huu haujawanufaisha wananchi wa Ileje kwa muda wote uliokuwa ukifanya kazi mpaka ulipofungwa:- (a) Je, ni lini mwekezaji mpya ataanza uzalishaji tena kwenye mgodi? (b) Je, ni lini tutakaa na mwekezaji huyu kama halmashauri ili kufahamiana? (c) Je, ni lini tutapata mwekezaji wa kutumia makaa haya kuzalisha umeme?

Supplementary Question 1

MHE. JANET Z. MBENE: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake, lakini naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, kwa kuwa kumekuwa na matamshi yanayotofautiana kutoka Serikalini kuhusiana na maendeleo ya mgodi huu, tungependa sasa kupata tamko rasmi ambalo wananchi watalielewa kuhusiana na uendelezwaji wa mgodi huu. Mwaka jana mwishoni tuliambiwa kuwa tayari mwekezaji ameshapatikana na karibu ataanza kazi. Tukaja kuambiwa mwekezaji yule ameonekana hafai na anatafutwa mwingine. Sasa tunaambiwa wako kwenye hatua za mwisho za kumtambulisha mwekezaji. Napenda kupata tamko rasmi kuwa ni lini huyo mwekezaji atapatikana na wananchi wategemee kuanza kufaidika na mgodi huo lini?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa mgodi huu umetolewa leseni kwa miaka 25 na kwa muda mrefu sana huu mgodi umekaa bure. Je, huo muda wa leseni utaongezwa pindi atakapopatikana huyo mwekezaji au la sivyo mategemeo ni yapi mwekezaji huyo akija?
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na suala la kwamba mgodi umechukua muda mrefu bila kuanza kazi zake, ni kweli kabisa. Labda nitoe historia kidogo ni kwamba Mgodi huu wa Kiwira ulikuwa uanze tangu mwaka juzi lakini mkandarasi aliyepatikana kwa ajili ya ujenzi huo baada ya kufanya upekuzi rasmi (due diligence) hakuonekana kuwa na uwezo wa kifedha. Kutokana na msimamo wa Serikali, tuliona tusitishe badala ya kuingia hasara kubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba baada ya pesa kupatikana sasa na kama mlivyoona tumepitisha shilingi bilioni mbili kwenye bajeti yetu na tunawashukuru sana Waheshimiwa Wabunge, tutaanza shughuli za awali ambazo zitahusisha pia ujenzi wa awamu ya kwanza pamoja na kuwalipa pia wakandarasi waliohusika katika feasibility study. Ujenzi kamili unatarajiwa kuanza Desemba 2017 au 2018 na utachukua miaka mingi kama inavyoonekana. Kwa hiyo, ujenzi wa mradi huu utaanza baada ya kumpata mkandarasi na matarajio makubwa mwaka 2018 utaanza kujengwa rasmi.

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, naona kwenye jibu langu nilijumlisha kwa harakaharaka. Labda nimweleze, ni kweli mgodi huu unachukua miaka 25 na miaka 25 ulikuwa ni uhai wa Mgodi wa Kiwira sawa na migodi mingine mikubwa hapa nchini. Sasa imechukua takribani miaka 11 wakati shughuli za upembuzi zinakamilika bila kuanza uzalishaji. Kwa utaratibu wa Sheria ya Madini Na. 14 ya 2010, kifungu cha 111, kama mwekezaji atagundua kwamba anahitaji kuongezewa muda anaweza pia kuongezewa uhai wa muda wa miaka 25 mingine mpaka atakapokamilisha shughuli za uchimbaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, uhai wa leseni, kama akiona reserve inatosha kuchimbwa na reserve iliyopo pale Kiwira ni tani milioni 30, kwa hiyo ni kweli kwamba tani milioni 30 inawezekana isichimbwe kwa ndani ya miaka 14 akahitaji muda mwingine mrefu. Akihitaji muda mwingine mrefu anaweza akaongezewa miaka mingine 25.

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. JANET Z. MBENE aliuliza:- Ileje inatambuliwa kuwa ndiyo inayokalia ardhi inayotoa makaa ya mawe yanayoitwa Kiwira Coal Mine lakini mgodi huu haujawanufaisha wananchi wa Ileje kwa muda wote uliokuwa ukifanya kazi mpaka ulipofungwa:- (a) Je, ni lini mwekezaji mpya ataanza uzalishaji tena kwenye mgodi? (b) Je, ni lini tutakaa na mwekezaji huyu kama halmashauri ili kufahamiana? (c) Je, ni lini tutapata mwekezaji wa kutumia makaa haya kuzalisha umeme?

Supplementary Question 2

MHE. PHILLIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kule jimboni kwangu, Jimbo la Songwe na wilaya mpya, kuna kampuni moja inaitwa Sun Marie, walipata leseni mwaka jana mwezi Aprili kwa ajili ya kuanza uchimbaji wa makaa ya mawe Kata za Magamba na Namkukwe Jimboni Songwe, lakini mpaka sasa hawaonekani walipo. Walikuwa wanafanya utafiti wa kujenga barabara mpaka sasa hatujajua wako wapi, Halmashauri haiwajui, tunaomba msaada wa Serikali, hawa watu kwanza wako wapi na ni lini wataanza kazi za uchimbaji wa madini haya?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kampuni anayoitaja Mheshimiwa Mulugo ipo katika eneo lake na kwa sasa hivi imepewa miaka saba kwa ajili ya kukamilisha utafiti. Miaka mitatu iliyobaki ya utafiti ni matarajio kwamba watakamilisha na waanze kuchimba rasmi. Kwa hiyo, nimwombe Mheshimiwa Mulugo avute subira ni matarajio baada ya miaka mitatu watakamilisha feasibility study na wataanza uchimbaji. Kwa hiyo,
baada ya miaka mitatu Mheshimiwa Mulugo atawaona wanakuja huko na magreda kwa ajili ya kuanza uchimbaji kama feasibility itaonesha kuna madini hayo

Name

Leonidas Tutubert Gama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Primary Question

MHE. JANET Z. MBENE aliuliza:- Ileje inatambuliwa kuwa ndiyo inayokalia ardhi inayotoa makaa ya mawe yanayoitwa Kiwira Coal Mine lakini mgodi huu haujawanufaisha wananchi wa Ileje kwa muda wote uliokuwa ukifanya kazi mpaka ulipofungwa:- (a) Je, ni lini mwekezaji mpya ataanza uzalishaji tena kwenye mgodi? (b) Je, ni lini tutakaa na mwekezaji huyu kama halmashauri ili kufahamiana? (c) Je, ni lini tutapata mwekezaji wa kutumia makaa haya kuzalisha umeme?

Supplementary Question 3

MHE. LEONIDAS T. GAMA: Mheshimiwa Naibu Spika, kule Songea kuna uchimbaji wa makaa ya mawe katika eneo Ngaka na uchimbaji wa makaa yale ya mawe unapita katika Mji wangu wa Songea. Kwa hiyo, pale Songea kuna uharibifu mkubwa sana wa mazingira kwa sababu yale magari yanayopita ni magari ya open body sio box body, matokeo yake ni kwamba mji unaharibika kimazingira lakini vilevile barabara zinaharibika. Nataka nijue Serikali ina mpango gani wa kuulipa fidia Mji wa Songea ili kukabiliana na majanga yanayotokana na usafirishaji wa makaa hayo ya mawe?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kama mnavyotambua, shughuli za uchimbaji wa madini zinaathiri mazingira kwa vyovyote vile hasa katika kusafirisha mitambo, kusafirisha madini lakini hata wakati wa uchimbaji. Nikubaliane na Mheshimiwa Gama kwamba kama kuna uharibifu wa mazingira kama ambavyo Sheria ya Madini inataja kwenye kifungu cha 65(1) (b) kwamba kama kutakuwa na uharibifu wa mazingira, Halmashauri inayohusika watakaa na mgodi kujadili uharibifu uliotokea kwa ajili ya kulipa fidia. Kwa hiyo, nimwombe Mheshimiwa Mbunge akae na Halmashauri yake, kama itadhihirika kwamba kuna uharibifu wa barabara unaosababishwa na kampuni hii basi wakubaliane suala la fidia kwa mujibu wa Sheria ya Madini pamoja na Sheria ya Ardhi.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pamoja na hayo, yapo majukumu mengine ya mgodi pamoja na Halmashauri. Nawashauri wakae wakubaliane juu ya tozo zinazoweza kutozwa kutokana na uharibifu wa mazingira. Hata hivyo, kabla ya mgodi kufungwa kwa kawaida kuna jambo linaitwa mine closure plan, hawa wamiliki wa leseni wana mine closure plan inayoonesha kwamba kama kuna uharibifu wa mazingira basi utafidiwa kulingana na uharibifu ulivyotokea.