Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 6 Energy and Minerals Wizara ya Madini 78 2016-09-14

Name

Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Primary Question

MHE. ABDALLAH H. ULEGA (K.n.y. MHE. MBARAKA K. DAU) aliuliza:-
Tafiti nyingi za mafuta na gesi zimefanywa na kampuni mbalimbali Kisiwani Mafia.
Je, ni nini matokeo ya tafiti hizo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbaraka Kitwana Dau, Mbunge wa Mafia kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kampuni za BP na Maurel Et Prome kwa nyakati tofauti zilifanya tafiti katika eneo la Kisiwa cha Mafia kukusanya takwimu za mitetemo kwa eneo lenye ukubwa wa kilometa za mraba 380 na 3D, lakini pia na katika Mkuza kwa kilometa 205 za 2D kuchimba visima viwili. Kati ya mwaka 1952 na 1956 kampuni ya BP ilichimba kisima cha Mafia -1 na kati ya mwaka 2006 hadi 2010 Kampuni ya Maurel Et Prome ilichimba kisima cha Mafia Deep -1. Baada ya tathmini ya takwimu hizo kufanyika matokeo yalionesha eneo hilo lina viashiria vya uwepo wa mafuta pamoja na gesi asilia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa leseni ya kitalu hicho imekwisha muda wake hivyo eneo hilo liko wazi kwa kampuni yoyote kuomba na kuendelea kazi ya uchimbaji mafuta na gesi katika eneo hilo.