Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Primary Question

MHE. ABDALLAH H. ULEGA (K.n.y. MHE. MBARAKA K. DAU) aliuliza:- Tafiti nyingi za mafuta na gesi zimefanywa na kampuni mbalimbali Kisiwani Mafia. Je, ni nini matokeo ya tafiti hizo?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH H. ULEGA: Mheshimiwa MWenyekiti, pamoja na majibu hayo mazuri ya Serikali, ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa Jimbo langu la Mkuranga utafiti ulishafanyika na ikagundulika gesi asilia katika kijiji cha Kiparang‟anda na kisima kiko pale. Naomba sasa Serikali inieleze ina mpango gani wa kuhakikisha kisima kile cha gesi kilichopo pale Mkuranga kinatumika kwa manufaa ya Taifa letu? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha gesi hii inatumika ipasavyo katika kuzalisha umeme wa uhakika ili kikidhi haja ya viwanda na makazi yanayokuwa kwa kasi katika Jimbo hili la Mkuranga? Ahsante

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa makampuni ya utafiti yamefanya utafiti wa mafuta na gesi katika maeneo mbalimbali hasa katika maeneo ya Pwani ikiwepo eneo la Kiparang‟anda. Nimhakikishie Mheshimiwa Ulega kwamba eneo la Kiparang‟anda bado linafanyiwa utafiti na kazi inayofanyika sasa ni kuthibitisha kama kweli gesi na mafuta vipo. Mara baada ya kuthibitika hatua itakayofuata ni appraisal kuangalia kibiashara kama mafuta hayo bado yanaweza kuchimbika. Hatua itakayofuata baada ya hatua hiyo ni eneo la kufanya uendelezaji yaani development na baada ya hapo sasa hatua inayofuata ni uchimbijaji wa mafuta. Kwa hiyo, nimshukuru sana Mheshimiwa Ulega, kazi inaendelea kufanyika na hatua zikifikia mwisho Mheshimiwa Ulega na wananchi wake watafahamishwa rasmi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili kuhusiana na manufaa ya gesi kutumika kwa ajili ya umeme. Ni kweli kabisa kwani kwa sasa asilimia kubwa ya umeme tunaotumia hapa nchini ni kutokana na gesi asilia. Ni vyema niwahakikishie wananchi pamoja Waheshimiwa Wabunge kwamba sasa hivi megawati 743 za umeme zinatokana gesi na ni kiasi kikubwa sana cha gesi. Kwa hiyo, wananchi wa Mkuranga na maeneo mengine ya Pwani na siyo Pwani tu Mtwara pamoja na Lindi hata maeneo mengine ya Ukanda wa Kaskazini tutaendelea kutumia umeme wa gesi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Ulega vijiji vyake pamoja na vijiji vingine vya Rufiji, vijiji ambavyo ni 42 pamoja na 43 vya Mheshimiwa wa Rufiji pamoja na Kibiti vyote vitapata umeme kwa kutumia umeme wa gesi.