Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 1 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 2 | 2025-01-28 |
Name
Zaytun Seif Swai
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza:-
Je, kuna mkakati gani wa kupeleka huduma za jamii na kuboresha miundombinu ya shule zilizobaki katika Tarafa ya Ngorongoro?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kupeleka huduma za jamii na kuboresha miundombinu ya shule katika maeneo yote yenye uhitaji, ikiwemo Tarafa ya Ngorongoro ambapo mwaka 2021/2022 hadi mwaka 2023/2024 Serikali imetumia jumla ya shilingi bilioni 7.9 za ruzuku ya elimu bila malipo katika Tarafa ya Ngorongoro. Aidha, mwaka 2024/2025, Serikali imetoa shilingi bilioni 1.7 za ruzuku ya elimu bila malipo, kwa ajili ya kuboresha huduma za elimu katika Tarafa hiyo.
Mheshimiwa Spika, vilevile halmashauri kupitia mapato ya ndani, mwaka 2024/2025 imetoa jumla ya shilingi milioni 120, kwa ajili ya kukarabati miundombinu katika katika Shule za Msingi Alailelai, Sendui, Olchanimerock, Naiyobi, Nainokanoka, Olbalbal, Ngoile, Moklal na Oloilob.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved