Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 1 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 4 | 2025-01-28 |
Name
Abdulhafar Idrissa Juma
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mtoni
Primary Question
MHE. ABDUL – HAFAR IDRISSA JUMA aliuliza:-
Je, lini Serikali itafanya ukarabati wa taa za barabarani zilizoharibika kwa kugongwa au hitilafu nyingine?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2024/2025, Wizara ya Ujenzi kupitia TANROADS imetenga fedha kiasi cha shilingi bilioni 1.8 kwa ajili ya kushughulikia masuala ya usalama barabarani ikiwemo kuweka na kukarabati taa za barabarani zilizoharibika kote nchini. Kwa sasa, TANROADS ipo katika hatua ya manunuzi ya kuwapata wakandarasi watakaofanya kazi hiyo. Baada ya kukamilika kwa hatua ya manunuzi na wakandarasi kupatikana, kazi ya ukarabati na uwekaji wa taa hizo itafanyika kulingana na mahitaji ya kila Mkoa. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved