Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 1 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 5 | 2025-01-28 |
Name
Dr. Thea Medard Ntara
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara kwa kutumia zege sehemu korofi ili kuepuka matengenezo ya mara kwa mara na upotevu wa fedha?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) imekuwa ikichukua hatua mbalimbali za kuboresha sehemu korofi katika barabara kama vile milima mikali, Mbuga na sehemu zenye udongo wa mfinyazi. Hatua hizo ni pamoja na ujenzi kwa kutumia zege, ujenzi kwa kutumia mawe na kadhalika. Pamoja na kuzingatia mahitaji, lakini pia uamuzi wa ujenzi wa aina gani utatumika kuzingatia gharama za upatikanaji wa mali ghafi za ujenzi zinazopatikana kwa urahisi katika eneo husika.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved