Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 2 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 21 | 2025-01-29 |
Name
Miraji Jumanne Mtaturu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Singida Mashariki
Primary Question
MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza:-
Je, lini Serikali itatenga fedha za kujenga Vituo vya Afya Kata za Misughaa, Issuna na Mang’onyi?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua uwepo wa kata ambazo hazina vituo vya afya kote nchini ikiwemo Kata za Issuna, Misughaa na Mang’onyi katika Jimbo la Singida Mashariki. Aidha, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali ilipeleka shilingi bilioni moja kwa ajili ya ujenzi wa Vituo vya Afya vya Ntuntu na Iglanson katika Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2025/2026 Serikali kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri ya Ikungi itatenga shilingi milioni 100 kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa kituo cha afya katika Kata ya Issuna. Kata za Misughaa na Mang’onyi zitajengewa vituo vya afya kwa awamu kwa kuzingatia mahitaji na vigezo vilivyoainishwa.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved