Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 4 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 53 | 2025-01-31 |
Name
Deo Kasenyenda Sanga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Makambako
Primary Question
MHE. BONIPHACE M. GETERE K.n.y. MHE. DEO K. SANGA aliuliza: -
Je, lini Serikali itaongeza Posho kwa Madiwani kwa kuwa wanafanya kazi kubwa kwenye Kata zao?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kazi kubwa inayofanywa na Waheshimiwa Madiwani katika kutoa huduma mbalimbali kwa wananchi.
Mheshimiwa Spika, kutokana na Halmashauri kuwa na uwezo mdogo wa mapato ya ndani ya kulipa posho za Waheshimiwa Madiwani, Serikali katika mwaka wa fedha 2021/2022, ilianza kulipa posho kwa Waheshimiwa Madiwani katika Halmashauri 168 kati ya 184 zilizopo. Katika kipindi cha mwaka 2021/2022 hadi 2023/2024 jumla ya shilingi bilioni 63.9 zimetolewa na Serikali kwa ajili ya kulipa posho za Madiwani.
Mheshimiwa Spika, posho za Waheshimiwa Madiwani bado hazikidhi mahitaji kutokana na Halmashauri nyingi kutokuwa na uwezo wa kulipa kupitia mapato ya ndani. Aidha, Serikali imeendelea kubuni vyanzo vya mapato ya ndani ya Halmashauri ili hatimaye posho za Waheshimiwa Madiwani na Wenyeviti wa Vijiji na Mitaa zilipwe kwa ufanisi zaidi.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved