Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 4 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 54 | 2025-01-31 |
Name
Grace Victor Tendega
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza: -
Je, ni upi mkakati wa Serikali kuhakikisha maeneo ya majiji na miji yanakuwa safi?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza mikakati mbalimbali kwa ajili ya kuhakikisha kwamba maeneo ya miji na majiji yanakuwa safi, ikiwa ni pamoja na kuendelea kutenga bajeti ya kuboresha miundombinu ya uondoshaji taka, ambapo katika kipindi cha mwaka 2021/2022 hadi 2023/2024 jumla ya shilingi bilioni 22.3 zilitengwa na shilingi bilioni 22.1 zilitumika. Aidha, shilingi bilioni 10.3 zimetengwa katika bajeti ya 2024/2025 kwa ajili ya shughuli za usafi wa mazingira katika majiji.
Mheshimiwa Spika, mikakati mingine ni pamoja na ushirikishwaji wa mamlaka mbalimbali za umma zenye wajibu kisheria wa kusimamia usafi ikiwemo TARURA na TANROAD, matumizi ya kampuni binafsi za usafi, uhamasishaji na utoaji wa elimu ya usafi wa mazingira kwa jamii, ushirikishwaji wa wadau katika kuanzisha vituo vya uchakataji na urejelezaji wa taka pamoja na utekelezaji wa sheria ndogo katika Mamlaka za Serikali za Mitaa.
Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kuwa pamoja na jitihada hizi, bado usafi wa baadhi ya miji hauridhishi. Hivyo, itaendelea kuhakikisha usafi unafanyika kikamilifu ili majiji na miji iwe kivutio kwa jamii na wageni pamoja na kuzuia magonjwa yatokanayo na uchafu.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved