Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 4 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 55 | 2025-01-31 |
Name
Esther Lukago Midimu
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. MINZA S. MJIKA K.n.y. MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza:-
Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Kituo cha Afya Sanga Mwalugesha, Wilaya ya Maswa?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 na 2023/2024 Serikali ilipeleka shilingi bilioni 1.9 katika Halmashauri ya Wilaya ya Maswa kwa ajili ya ukarabari wa hospitali pamoja na ujenzi wa Vituo viwili vya Shishiyu na Badi. Aidha, ujenzi na ukarabati wa hospitali ya wilaya pamoja na vituo vya afya umekamilika na vinatoa huduma.
Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya katika kata za kimkakati zilizokidhi vigezo ikiwemo Kata ya Sanga Mwalugesha.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved