Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 18 Sitting 4 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 56 2025-01-31

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuondoa tope lililojaa katika Bwawa la Kalemawe – Same?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imechukua hatua mbalimbali ili kuhakikisha inaondoa tope lililojaa katika Bwawa la Kalemawe – Same ikiwa ni pamoja na kukamilisha kazi ya usanifu wa kina na kuandaa gharama kwa ajili ya ukarabati wa bwawa hilo kwa kuondoa tope, kukarabati utoro wa maji, kujenga msingi wa tuta na tuta la bwawa.

Mheshimiwa Spika, pia, Serikali kupitia Wizara ya Maji imetenga fedha, shilingi bilioni moja, ambapo ukarabati umepangwa kufanyika katika robo ya nne ya mwaka wa fedha 2024/2025, nakushukuru.