Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuondoa tope lililojaa katika Bwawa la Kalemawe – Same?

Supplementary Question 1

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Spika, nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa kazi hii ya kutoa tope katika Bwawa hili la Kalemawe imechukua miaka mingi sana na hivyo kuathiri kazi za kiuchumi za Wilaya ya Same hasa Jimbo la Same Mashariki kwa upande wa uvuvi na umwagiliaji, je, Waziri anaweza kuniambia kwamba anakadiria kazi hii itachukua muda gani? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Kwa kuwa wananchi wa Wilaya ya Same wanataka wawe na uhakika kwamba kweli kazi hii inafanyika, je, Serikali iko tayari kunisaidia nipate andiko hili la usanifu wa kina ili niweze kuwa na ushahidi kwamba kweli kazi hii itakwenda kufanyika? Ahsante. (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama tulivyoeleza katika jibu la msingi kwamba kazi hii imepangwa kufanyika katika robo ya nne ya mwaka huu wa fedha, tunaendelea kumwambia Mheshimiwa Mbunge aendelee kuwa na subira. Wizara inaendelea kupambana kuona namna ambavyo tunakamilisha kazi hii na kuhakikisha kwamba wananchi wanaendelea kuondokana na changamoto hii.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa tunataka tuwaridhishe wananchi ambao ndio wanapata changamoto kubwa ya kuenea na kuwepo kwa tope katika bwawa hili, na kwa kuwa tunataka tumpatie nafasi Mheshimiwa Mbunge cha kwenda kuzungumza kwa wananchi, tupo tayari na tutampatia hayo maelezo au hiyo taarifa ili naye aweze kujiridhisha na kazi iweze kuendelea, nakushukuru.

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuondoa tope lililojaa katika Bwawa la Kalemawe – Same?

Supplementary Question 2

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Hili swali limeulizwa hapa Bungeni mara nyingi sana, na majibu yanayotolewa na Serikali ni haya haya. Naomba nimwambie Mheshimiwa Waziri kitu kimoja, naomba leo anambie ni lini atakwenda kuliona lile Bwawa la Kalemawe ili wananchi waamini kwamba Serikali iko serious? Ahsante.

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mama Anne Kilango kwa kumwahidi kwamba mara tu baada ya kukamilika kwa Bunge hili, nitahakikisha kwamba tunafuatana pamoja kwenda katika hilo eneo ili kuona changamoto na kuona namna ambavyo tunaweza tukawasaidia wananchi wa eneo hilo, nashukuru.