Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 4 | Enviroment | Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano | 58 | 2025-01-31 |
Name
Kenneth Ernest Nollo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bahi
Primary Question
MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka Sheria kabambe kudhibiti uharibifu wa mazingira nchini?
Name
Khamis Hamza Khamis
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Uzini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -
Mheshimiwa Spika, katika kudhibiti uharibifu wa mazingira na kutatua changamoto mbalimbali za kimazingira nchini, Serikali imetunga na inatekeleza Sheria ya Usimamizi wa Mazingira Sura ya 191 ambayo inasimamia masuala yote yanayohusiana na mazingira nchini Tanzania. Sheria hii imeweka msisitizo wa udhibiti wa uharibifu wa mazingira kwa kukataza uchafuzi wa maji, hewa, na udongo kupitia kemikali za viwandani, kilimo, na shughuli nyingine za kibinadamu.
Mheshimiwa Spika, aidha, imeweka msisitizo kwa miradi yote mikubwa kwamba ni lazima ifanyiwe tathmini ya awali ya athari za mazingira kabla ya mradi kuanza ili kuepuka uharibifu wa mazingira. Pia, sheria inahimiza wananchi kuhamasishwa kushiriki katika uhifadhi na usimamizi kupitia elimu, sheria ndogo ndogo za Serikali za Mitaa, na mipango ya uhifadhi wa mazingira, nashukuru.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved