Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 4 | Health and Social Welfare | Wizara ya Afya | 59 | 2025-01-31 |
Name
Bonnah Ladislaus Kamoli
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Segerea
Primary Question
MHE. MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza:-
Je, hatua gani za kinidhamu zimechukuliwa kwa madaktari wanaoendelea kuzuia Maiti kutokana na deni la matibabu kinyume na maelekezo ya Serikali?
Name
Dr. Godwin Oloyce Mollel
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Siha
Answer
NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -
Mheshimiwa Spika, maiti huwa zinazuiliwa na uongozi wa hospitali zetu na wala siyo suala la madaktari. Katika maeneo ambayo tumefanya ufuatiliaji ili kuchukua hatua za kinidhamu kwa viongozi husika, tumebaini ndugu wa marehemu ndio waliokataa kufuata utaratibu uliowekwa kwa nia ya kuzuia hoja za ukaguzi. Badala yake, ndugu hao walikimbilia kulalamika kwenye vyombo vya habari na kwa viongozi, hasa Wabunge.
Mheshimiwa Spika, ni kweli Serikali ilishatoa maelekezo kwa vituo vyote vya kutolea huduma za afya nchini kupitia Waraka Na. 1 wa Mwaka 2021 wa kutozuia maiti na kuweka utaratibu wa kulipia gharama za matibabu na madeni ya miili.
Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved