Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 4 | Health and Social Welfare | Wizara ya Afya | 60 | 2025-01-31 |
Name
Fatma Hassan Toufiq
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. FATMA H. TOUFIQ aliuliza: -
Je, watoto wa kike wangapi na wanawake wangapi walioathirika na utoaji mimba usio salama nchini?
Name
Dr. Godwin Oloyce Mollel
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Siha
Answer
NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -
Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2024 idadi ya wanawake na wasichana waliopata changamoto ya kuharibikiwa na mimba na kupata huduma katika vituo vya huduma za afya ni kama ifuatavyo: -
(i) Wanawake na wasichana 181,071 ambao walipatiwa huduma na kuruhusiwa kama wagonjwa wa nje (outpatients);
(ii) Wanawake na wasichana 32,512 ambao walipatiwa huduma wakiwa wamelazwa (inpatients).
Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka 2022 hadi 2024, wanawake 92 walipoteza maisha kutokana na changamoto mbalimbali zinazosababishwa na kuharibika kwa mimba.
Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved