Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 4 | Finance and Planning | Wizara ya Fedha | 61 | 2025-01-31 |
Name
Janeth Elias Mahawanga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. JANETH E. MAHAWANGA aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha jamii inapata uelewa kuhusu umuhimu wa kulipa kodi na kudai risiti?
Name
Hamad Hassan Chande
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kojani
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA alijibu: -
Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali ili kujenga uelewa kuhusu umuhimu wa kulipa kodi na utoaji wa risiti za mauzo na ununuzi wa bidhaa na huduma. Hatua zinazochukuliwa na Serikali ni pamoja na: -
(i) Kutoa elimu elimu ya kodi kwa njia mbalimbali ikiwemo redio, runinga, mitandao ya kijamii, makongamano, maonesho ya biashara ya Kitaifa, Kimataifa na semina;
(ii) Kuwatembelea wafanyabiashara katika maeneo yao mlango kwa mlango, kutoa elimu inayoainisha wajibu wa mlipakodi kwa TRA na wajibu wa TRA kwa mlipakodi kupitia mkataba wa huduma kwa mlipakodi;
(iii) Kuanzisha huduma za bure ikiwemo namba za simu za bure zinazowezesha walipakodi kuwasiliana na Ofisi za TRA moja kwa moja; na
(iv) Kuanzisha ofisi zinazotembea (Mobile Tax Offices) ambazo zinatumika kama ofisi kamili kwa ajili ya kutoa elimu ya kodi kwa umma na kusajili walipakodi wapya, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved